Na Steven Augustino,
Tunduru
MKUU wa Wilaya ya Tunduru, mkoani
Ruvuma, Chande Nalicho ametoa wiki moja kwa wakulima na wafugaji wa jamii ya
Kisukuma kuondoka katika eneo la hifadhi ya msitu wa Shamba la bibi vinginevyo hatua
kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao
.Nalicho alitoa
agizo hilo
baada ya Kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo kufanya ziara ya kushtukiza
katika msitu huo na kujionea hali halisi ya uharibifu wa vyanzo vya maji na
misitu iliyopo katika hifadhi hiyo inayounganisha Vijiji vya Nangunguru, Majala
na Mkalekawana katika Tarafa ya Nampungu Kata ya Nandenbo wilayani humo.
"Natoa
siku saba kwa watu wote waliovamia msitu huu wa hifadhi waondoke, haiwezekani
watu waendelee kuishi wanavyopenda na kuharibu mazingira katika vyanzo vya maji
na hifadhi ya misitu kana kwamba Serikali haipo," alisema
Alisema katika
kutekeleza agizo hilo kwa watakao kaidi amri
hiyo ofisi yake itatumia sheria Namba 24 kifungu cha 16 kinachompa mamlaka ya
kuharibu makazi au mali
baada ya mhusika kukataa kutekeleza amri halali ya iliyotolewa na mamlaka
husika.
Pamoja na kutolewa
kwa amri hiyo dhidi ya wakulima na wafugaji hao DC, pia aliwataka watendaji
kata na vijiji kwa kushirikiana na maofisa Tarafa wilayani humo kutekeleza majukumu
yao ikiwemo
kuwaelekeza wafugaji
kufuata taratibu za
kuonana na viongozi wa vijiji husika, kufanya mikutano inayo wahusisha wananchi
katika maamuzi ya kuwapokea wafugaji hao ili kuyaondoa maeneo yao katika migogoro ya aina hiyo.
"Kwavile mifugo ni
muhimu kwetu na endapo itatumika vizuri na kwa kuzingatia kanuni, miongozo na
maelekezo yanayotolewa na Serikali, italeta manufaa kwa
Wananchi wetu,"
alisema Nalicho na kuongeza kuwa mtindo wa kuishi kwa uhasama kati ya wafugaji
na wakulima hauwezi kuwa na tija.
Awali akizungumza
katika ziara hiyo Ofisa misitu wa Wilaya ya Tunduru, Rashid Mtotela alimweleza
mkuu huyo wa wilaya kuwa wakulima na wafugaji hao waliuvamia msitu huo mwaka
2006 /2007 na kuendelea kujiimarisha kila mwaka baada ya kubaini kutokuwepo kwa
vikwazo vyovyote kutoka serikalini.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Nangunguru, Said Rashid Mkwekwele, Mtendaji wa
Kijiji hicho, Zainabu Twaha na Ofisa Tarafa wa Nampungu, Joshua John
waliwalaumu baadhi ya wakuu wa Idara katika halmashauri ya wilaya hiyo kuwa
umekuwa na kigugumizi katika ufuatiliaji na uchukuaji wa maamuzi juu ya
migogoro hiyo
No comments:
Post a Comment