Na Elizabeth Joseph, Dodoma
SERIKALI imesema kuwa itawachukulia
hatua kali za kisheria wale wote wanaojihusisha na biashara haramu kwa watoto
wanaoishi katika mazingira magumu na yatima.Tamko hilo lilitolewa juzi mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Rehema
Nchimbi wakati akihutubia katika hafla ya watoto yatima na wanaoishi katika
mazingira magumu.
Dkt. Nchimbi
alisema kuwa kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu kutumia mwanya wa maisha ya
watoto hao kuwafanyisha biashara ya dawa za kulevya pamoja na ukahaba jambo
ambalo ni kuwanyima haki zao watoto na kuwanyanyasa.Aliongeza kwa
kuwataka watu hao kuanza kuwatumia watoto, mke, mume ama familia zao katika
biashara hizo ili wajue endapo kuna raha ama karaha kwa kufanya vitendo hivyo.
"Wauzaji wa dawa
za kulevya na wanaowatumia watoto hawa kuwafanyisha biashara hizo waanze na
watoto ama wake zao ili wajue uchungu au kama
kuna raha yoyote kwa kuwafanyia hivyo," alisema Dkt. Nchimbi.
Aidha aliwataka
viongozi wa siasa nchini hasa wanaoishi mkoani hapa kutothubutu kuleta vurugu
za kisiasa zitakazoweza kuvuruga amani ya wananchi pamoja na maisha yao kwa ujumla.
Dkt. Nchimbi pia
aliwataka watu wenye uwezo wa mali
kutumia mali zao kuwasaidia
watoto hao kwakuwa wengine kati yao
ndiyo chanzo cha kupatikana kwa watoto hao kwa kutumia pesa zao katika anasa na
kuwatelekeza watoto hao.
Kwa upande wake
Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mustapha Musa Rajabu aliwataka viongozi wa dini
nchini kutowadharau watu wasiojiweza pamoja na kuwataka watu ama makampuni yenye
mali kuacha tabia ya kukumbatia mali zao wakati kuna jamii inayohitaji
kusaidiwa kwa kuwapa chakula, mavazi, elimu na mambo mengine.
Naye Mwenyekiti wa
kamati ya hafla hiyo, Faustine Mwakalinga alisema kuwa waliamua kufanya sherehe
hiyo ili kukaa na kufurahi kwa pamoja na watoto hao na kuitaka jamii kuchukua
jukumu la kubadili mazingira magumu ya watoto hao na kuyafanya mazuri na yenye
hadhi.Jumla ya watoto 420
walishiriki katika hafla hiyo walitoka katika vituo mbalimbali vya kulelea
watoto pia hafla hiyo ilidhaminiwa na makampuni ya simu za mkononi pamoja na
Aza
No comments:
Post a Comment