19 July 2013

WIZI WA UMEME KIMEELEWEKA



 Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Temeke limethibitisha kuwa Kituo cha Polisi Tandika, Azimio (Vyaniza) jijini Dar es Salaam, kimekuwa kikiibia Serikali malipo ya ankara za umeme kutokana na hujuma iliyofanyika kituoni hapo kwa kuwaunganishia umeme baadhi ya wafanyabiashara kinyume cha sheria. Hayo yalithibitishwa jijini Dar es Salaam jana na Meneja wa TANE S CO Mk o a wa Temeke, Richard Mallamia, wakati akizungumza na maofisa waliotumwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ili kujiridhisha kuhusiana na hujuma hiyo kutokana na habari iliyochapishwa na gazeti la Majira, Jumamosi iliyopita.


Mallamia aliwaambia maofisa hao kuwa ni kweli umeme umekuwa ukiibiwa kupitia kituoni hapo na kusambazwa kwa wafanyabiashara (majina tunayo). Kwa mujibu wa uchunguzi wa Majira, wafanyabiashara hao kila mwezi walikuwa wakilipa sh. 30,000 kwa kituo hicho na kuingia kwenye mifuko ya waliohusika kusuka mpango huo. " Tume t h i b i t i s h a umeme umekuwa ukisambazwa kinyume cha taratibu kwa wafanyabiashara, lakini tunaoibiwa sio TANESCO bali polisi wanaiibia Serikali ambapo wizara husika inatumia fedha za walipa kodi kulipa bili za umeme za Jeshi la Polisi," alisema.

Alifafanua kwamba kitendo cha polisi kuwasambazia umeme wafanyabiashara hao ni hatari kwakuwa waya umepitishwa chini ya ardhi, jambo ambalo linaweza kusababisha maafa makubwa kwa wapita njia.

Wakati wawakilishi hao wa waziri wakifanya ukaguzi kituoni hapo na kwenye maeneo ya biashara walikuta tayari mfumo wa kusambaza umeme uliokuwa umeunganishwa awali umefumuliwa ili kuficha ushahidi.

Hata hivyo maofisa hao baada ya kufuatilia kwa undani walibaini kufanyika hujuma hiyo, huku baadhi ya wafanyabiashara waliokuwa wame u n g a n i s h iwa umeme wakishikwa kigugumizi kujibu maswali waliyokuwa wanaulizwa.

Mmoja wa watu wanaotajwa kuhusika kwenye hujuma hiyo (jina tunalo) alipoulizwa na maofisa hao kutoka wizarani alikataa hujuma hiyo kufanyika. Lakini alipooneshwa jinsi hujuma hiyo ilivyokuwa ikifanyika baada ya kuchimba chini ya ardhi na kukuta waya unaotoka kituoni hapo na kuingia kwa wafanyabiashara hao, alipatwa na kigugumizi na kuanza kutokwa machozi.

Mkuu wa kituo hicho, Mohamedi Jaf Khamisi, alipoulizwa na maofisa hao, alisema ana wiki tatu tangu ahamishiwe kituoni hapo, hivyo hafahamu kitu chochote.

Aliongeza kuwa tayari taarifa za suala hilo ameziandikia maelezo na kuziwasilisha kwa Kamanda wa Mkoa wa kipolisi Temeke, Engelbert Kiondo.

Kwa upande wake Kamanda Kiondo, alisema ana ripoti iliyoandaliwa na wahandisi wa TANESCO waliokwenda kukagua awali mara baada ya taarifa hiyo ya wizi wa umeme kuchapishwa gazetini ambayo haioneshi tuhuma zozote za kuibwa umeme katika kituo hicho.

"Uc h u n g u z i u l i o f a n ywa na wahandisi wa TANESCO haukuonesha kasoro zozote, na hivi sasa jalada lake linakaribia kukamilika, hivyo sisi tunaifanyia kazi ripoti hiyo," alisema na kuongez a; " hiyoripo tinyin gine(yamaofisawawaz iri)nd iyokwa nza naisikia kutoka kwako.".

NayeMkaguzi kutoka Kanda ya Pwan i, Ch ristian Simon, alisema kituochapolisikinauzaumemewakati wiz arainap ata hasarakwa kulipabiliamb ayosiosahihi.

Ali semawames hawa andi kiafomuya u kaguzikwaajiliya kuangalia mfumo wa bili halafu hatua stahiki zitafuata.

1 comment:

  1. HAO NDIYO POLISI WETU CHEZEA POLISI WEWE!
    BAADHI YA POLISI NI HATARI KULIKO MARALIA

    ReplyDelete