London,
Uingereza
WASHIKA bunduki wa Kaskazini mwa London
nchini England, klabu ya Arsenal wamejipanga tena kutuma ofa ya pauni milioni
35 wiki hii ili kuinasa saini ya mshambuliaji wa klabu ya Liverpool, raia wa
Uruguay, Luis Suarez.
Suarez amekuwa
chaguo namba moja kwa kocha wa Arsenal majira haya ya kiangazi ya usajili
barani Ulaya, Mfaransa, Arsene Wenger na sasa anaandaa kitita hicho ingawa
Liverpool walisema kama anataka kumsajili nyota huyo anatakiwa kulipa ada ya
uhamisho ya pauni milioni 40.
Awali Wenger
alituma ofa ya pauni milioni 30 na Liverpool wakakataa, sasa wiki hii ameongeza
pauni milioni 5 na kufikia 35, lakini sijui kama Liver watakubali kwani
walishasema wanahitaji 40 na si vinginevyo.
Mashabiki wa
Arsenal wana imani kubwa kuwa mshambuliaji huyo mwenye matatizo makubwa nchini
England ataweza kuwasili Emirates, na wanataka kitita cha pauni milioni 70
alichopewa Wenger kwa ajili ya usajili kitumike kumleta Kaskazini mwa London.
Wenger yupo katika presha kubwa
ya kusajili wachezaji wenye vipaji vya hali ya juu kutokana na klabu hiyo
kusema kuwa kwa sasa ina uwezo wa kushindana katika soko la kutafuta wachezaji
ghali zaidi duniani.
No comments:
Post a Comment