24 July 2013

WAWEKEZAJI WA MADINI WATAKIWA KULIPA KODI


Na Pamela Mollel, Arusha

 KAMPUNI za madini hapa nchini zimetakiwa kulipa kodi ikiwemo ile ya faida ili Serikali iweze kupeleka huduma za msingi katika maeneo yaliyopo pembezoni mwa migodi.M a e n e o a m b a y o yalielezwa kwa asilimia kubwa yameachwa nyuma kimaendeleo. Hali hiyo inadaiwa inatokana na kampuni nyingi pindi zinaporidhia kuwekeza katika maeneo hayo kuahidi mambo mbalimbali ikiwemo ujenzi wa barabara, vituo vya afya na maji bila mafanikio
. Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni jijini Arusha na mwakilishi wa Kamati ya Utekelezaji Kupitia Taasisi ya Tanzania Extractive Industry Tranparent Initiative (TEITI), Buberwa Kaiza kwa niaba ya Jaji Mark Bomani wakati akizindua ripoti ya utafiti wa uwajibikaji wa makampuni kwa jamii ya sekta ya madini hasa Tanzanite.
Buberwa alisema kuwa, kama makampuni ya madini yangekuwa yanalipa kodi basi serikali ingepata fursa kupeleka huduma zote muhimu ikiwemo kujenga barabara, hospitali, shule huku akidai kuwa eneo kama Mererani lisingekuwa maskini ilhali linatoa madini ya Tanzanite.
"Ripoti iliyofanyika katika Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mererani na kuwashirikisha wachimbaji wadogo wadogo wengi wamelalamikia ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na wawekezaji kama kuwafungulia maji ndani ya mashimo, kuuawa kwa wachimbaji," alisema Buberwa.
Alisema kuwa, katika ripoti moja ya kamati hiyo kuna kampuni moja ya madini haikulipa kodi kutokana na kudai kuwa ilipata hasara hivyo inafidia kwanza hasara ndiyo ilipe kodi jambo ambalo alisema huwezi kulikuta katika nchi za wenzetu.
Kwa upande wake Katibu wa Muungano wa Asasi Zisizo za Kiserikali Arusha Angonet, Peter Bayo ambayo ndiyo waandaaji wa ripoti hiyo alisema kuwa, utafiti huo umechukua takriban miezi 3 na ulifanyika Mererani.
Alisema kuwa, kubwa katika utafiti huo ni kutengeneza mfumo wa kuwezesha uwajibikaji wa kampuni kwenye jamii ikiwa ni pamoja na jamii kunufaika na rasilimali zinazopatikana.
"Uwe p o wa uwa z i katika mikataba pamoja na mapato kuwa ni kiasi gani kinapatikana...wananchi wanahaki ya kufahamu hayo yote," alisema Bayo
Pia alieleza lengo la utafiti huo kuwa ni kuangalia hali ya mchango wa shughuli za uchimbaji wa madini aina ya Tanzanite katika maendeleo ya jamii, uhifadhi na utunzaji wa mazingira, usalama wa haki za binadamu na uwazi katika masuala ya kodi.
Mmoja wa waalikwa katika uzinduzi huo ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika lisilokuwa la kiserikali la Hakimadini, Amani Mhinda akichangia mada alisema kuwa utafiti huo ni muhimu sana na umekuja wakati ambapo kuna mjadala mkubwa kuhusu jinsi gani nchi ya Tanzania itafaidika na rasilimali zake
"Utafiti huu unatoa ushahidi kwa wananchi na serikali za mitaa kufahamu athari za uwekezaji ili kushawishi serikali kuu kuboresha sera za uwekezaji katika sekta ya madini," alisema Mhinda.

No comments:

Post a Comment