17 July 2013

WATANO WAJERUHIWA AJALI YA SCANIA NA FUSO


 Na Damiano Mkumbo, Singida
WATU watano wamejeruhiwa baada ya magari mawili kugongana katika kijiji cha Kitukutu, Tarafa ya Kinampanda wilayani Iramba Mkoa wa Singida barabara Kuu ya Singida Nzega.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela alieleza kuwa watu hao walijeruhiwa katika ajali hiyo Julai 14 baada ya gari aina ya Scania T 922 BUC/T539 BUH kugongana na Fuso T 748 BCM.
Kamwela aliwataja majeruhi hao ambao wote wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Iramba Kiomboi kuwa ni pamoja na Mustafa Mohamed (43),mkazi wa Sanya juu, dereva wa Fuso na Msilumi Emmanuel (21) mkazi wa Ubungo Dar es Salaam, wote wakiwa na majeraha usoni.

Alisema wengine ni Swalehe Idd (21), utingo wa Fuso mkazi wa Kilimanjaro aliyevunjika miguu yote miwili na kuwa na majeraha usoni, Leila Mohamedi (40), mkazi wa Chanika Dar es Salaam na Aley Simba (32) wa Mbezi Beach ambao wote wamepata maumivu na michubuko mikononi, mabegani, kifuani, kiunoni na miguuni.
Akizungumza kuhusu ajali hiyo na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Kamanda Kamwela alibaini kuwa lori hilo lililokuwa likiendeshwa na Nicodemus Hanery lilitokea Uganda kuelekea jijini Dar es Salaam wakati gari jingine aina ya Fuso lilikuwa likiendeshwa na Mustafa Mohamed lilitoka Dar es Salaam kwenda Mwanza.
"Chanzo cha ajali ni mwendokasi wa dereva wa Fuso ambaye alijaribu kupishana na lori hilo lililokuwa na trela kati sehemu isiyoruhusiwa kitendo kilichosababisha magari hayo kugongana uso kwa uso."
Aliongeza kuwa majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Kiomboi na hali zao zinaendelea vizuri na dereva wa Fuso yupo chini ya ulinzi na anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara taratibu zitakapo kamilika.
"Kutokana na tukio hilo nina washauri madereva wanapokuwa barabarani kuendesha magari yao kwa kuzingatia sheria za usalama wa barabarani na kuwajali watumiaji wengine wa barabara

No comments:

Post a Comment