Na Masanja Mabula, Pemba
WAKAZI wa Shehia ya
Msuka katika Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba wameingiwa na hofu juu
ya usalama wa nyumba zao baada ya maji ya bahari kuendelea kuvamia nchi kavu
kwa kasi siku hadi siku. Wakizungumza jana katika eneo la bandari Msuka walisema kuwa
kutokana na hali ya mawimbi ya bahari kuzidi kuitafuna nchi kavu, hivyo
wamekuwa na hofu kubwa ya kukosa sehemu ya kuishi kwa siku za baadaye
. Suleiman Assaa Khamisi alisema kuwa kwa kipindi cha miaka mitano
iliyopita bahari katika eneo hilo inakisiwa kuwa imechukua eneo lenye urefu wa
mita 25 na kusababisha miti mingi ikiwemo minazi kupotea. Aidha, amefahamisha kwamba kutowekwa kwa miti hiyo ambayo kwa sasa
imebakia visiki huku baadhi ya mingine ikiwa imetoweka kabisa kwa kung'oka na
hivyo kuongeza mmomonyoko ya ardhi katika eneo hilo.
Naye Masahare Nassor Masahare akizungumza na mwandishi wa habari
hizi ameitaka Serikali kuangalia uwezekano kuwasaidia katika kutafuta mbinu na
njia za kuzuia kazi ya maji ili isiendelee kuyasogelea makazi yao. Alisema kuwa licha ya tatizo hilo kujulikana na baadhi ya viongozi
wa Jimbo, lakini bado juhudi za kulitafutia ufumbuzi hazijaonekana.
Ka t i b u wa B a n d a r i y a Msuka Mjawiri Rashid Bakar
akizungumzia suala hilo amesema kuwa wamekuwa wakichukua hatua za kupambana na
tatizo hilo , lakini juhudi zao zimeshindwa kuleta mafanikio. Alizitaja baadhi ya hatua ambazo uongozi wa bandari umezichukua
katika kukabiliana na hali hiyo kuwa ni pamoja na kupanda miti kandokando ya
bahari na kuweka viroba vyenye mchanga sungo sungo ili kuzuia hali hiyo. Mjawiri alieleza kwamba, iko haja kwa serikali kuelekeza
nguvu zake katika eneo la Bandari ya Msuka kwa kuhakikisha kwamba inajenga
ukuta ili kuzuia maji ya bahari yasiendelee kuyavamia makazi ya watu.
No comments:
Post a Comment