Na Patrick Mabula, Kahama
MA K A M U Mwenyekiti
wa Halmashauri ya Ushetu, wilayani Kahama, Tabu Katoto amewa t a k a wa n a n c
h i wa s i bwe t e k e k a t i k a kuchangia huduma za kijamii ili kuharakisha
maendeleo. Wito huo aliutoa wiki iliyopita katika harambee ya kuchangia
ujenzi wa vyumba vya madarasa na nyumba za walimu katika sekondari ya Kata ya
Igunda ambapo wananchi wa kata hiyo waliweza kuchanga kiasi cha shilingi milioni
10.5.
Katoto aliwataka wananchi kuendelea kuwa na moyo wa kuchangia
maendeleo katika huduma za kijamii hali itakayosaidia kuharakisha maendeleo
kwenye maeneo yao.
Katoto ambaye ni Diwani wa Kata ya Igunda ambayo haina shule ya
sekondari aliwapongeza wananchi kwa hatua waliyofikia ya kujenga na kukamilisha
vyumba vitatu vya madarasa na nyumba moja ya mwalimu kwa nguvu zao ambavyo hadi
sasa wametumia kiasi cha shilingi milioni 18 .
Kwa upande wake mgeni rasmi katika harambee hiyo Mbunge wa Jimbo
la Kahama, James Lembeli aliyechangia kiasi cha shilingi milioni tatu na bati
100 kwa ajili ya kuezeka boma la nyumba ya walimu iliyojengwa kwa nguvu ya
wananchi. Akiongea katika harambee hiyo Lembeli alitoa onyo kwa watendaji wa
vijiji na kata kuacha mara moja kuchakachua na kutafuna michango ya wananchi
hali ambayo imekuwa ikiwavunja moyo na kuwakatisha tamaa katika suala la
kujiletea maendeleo.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ushetu, Juma Kimisha
katika kuunga mkono jitihada hizo za wananchi, alitoa jumla ya mifuko ya saruji
15, huku ofisa toka ofisi ya CAG, Elias Kuandikwa ambaye ni mzaliwa wa kata
hiyo aliwachangia kiasi cha shilingi milioni moja taslimu.
No comments:
Post a Comment