23 July 2013

WANAFUNZI 10 WA JIOLOJIA UDSM WAPATA UDHAMINI



Na Darlin Said

WANAFUNZI 10 wa Kitivo cha Jiolojia katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), wamepata udhamini wa masomo ya shahada ya kwanza chuoni hapo kwa lengo la kuongeza wataalam wa masuala ya madini na mafuta nchini.

Udhamini huo kwa wanafunzi hao umetolewa na kampuni inayojishughulisha na masuala ya mafuta na gesi ya Swala Oil and Gas Tanzania Limited (Swala) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo, Dkt. David Ridge,wakati akitangaza udhamini huo ambao ulitangazwa Juni, mwaka huu.

"Tumefurahi kupata wanafunzi h awa amb a o t u n a t a r a j iwa kuwadhamini waliojitokeza kuomba msaada wetu walikuwa wengi ila tumezingatia wale waliofaulu kwa kiwango cha juu katika matokeo yao ya kidato cha sita katika masomo husika," alisema Dkt. Ridge.

Aliwataja wanafunzi hao kuwa pamoja na Joel Haule, Robert Kisimbo, Andrew Marong, Denis Muhoka, Rafael Ngole, Levina Pangani, Lucy Pangani, Emmanuel Rajabu, Anita Ringia na John Sospeter.

Naye Mkuu wa Idara ya Jiolojia UDSM, Dkt. Shukrani Manya, alisema msaada uliotolewa na Kampuni ya Swala kwa wanafunzi hao utasaidia kusoma na kufanikiwa kupata shahada yao ya kwanza.

"Ms a a d a h u u mb a l i n a kuwawezesha kupata shahada yao ya kwanza, pia utasaidia katika kuwajengea uwezo wao hasa katika masuala ya mafuta na gesi katika sekta ndogo ndogo ambako ndio maendeleo ya Watanzania yanapotokea," alisema.

Alisema uamuzi wa kampuni hiyo utasaidia kujenga ushirikiano baina ya vyuo vikuu vya Tanzania na sekta binafsi za madini.

No comments:

Post a Comment