24 July 2013

WANACHAMA SIMBA WAMSHTAKI RAGE TFF



 Na Fatuma Rashid
WANACHAMA wa Klabu ya Simba, wamewashtaki v i o n g o z i wa o kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kutaka wapewe adhabu kwa madai kwamba wamevunja kanuni za Mkutano Mkuu wa mwaka.Mkutano huo ulifanyika wiki iliyopita katika Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay, Dar es Salaam.

Hata hivyo, mkutano huo uliingia dosari, baada ya baadhi ya wanachama kupinga ajenda ya mpango mkakati wa maendeleo ya klabu hiyo, ingawa Mwenyekiti wa Simba Aden Rage alifanikiwa kuzima vurugu hizo kwa kushirikiana na polisi na mabaunsa.Akizungumzia sakata hilo Dar es Salaam Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alisema amepokea barua kutoka kwa baadhi ya wanachama wa klabu ya Simba, wakilitaka shirikisho hilo kuwaadhibu viongozi wa klabu wakidai viongozi hao wamevunja masharti ya mkutano huo.
Lakini Osiah alisema TFF aihusiki kwa lolote katika hilo na wanashangaa kupelekewa mzigo na wanachama kutaka kuwaadhibu viongozi wao.“Klabu yoyote inapokuwa na mkutano, TFF hatuhusiki sasa linapokuja suala la kutokuelewana tunashangaa tunapopewa mzigo na wanachama, ili tuwaadhibu viongozi wao,” alisema.
Aliongeza kuwa wanachama hao inawabidi waombe Mkutano wa Dharura, ili waweze kuelewana vizuri na viongozi wao na kama wakishindwa kuelewana, basi waangalie katiba inasemaje.Katika mkutano huo uliofanyika muda mfupi, Rage aliwaahidi wanachama wa Simba hasa waliokuwa wakiupinga uongozi wake kwamba wataitisha mkutano wa dharura Novemba mwaka huu pamoja na kuzungumzia kuuzwa kwa Emmanuel Okwi nchini Tunisia.

No comments:

Post a Comment