Na Suleiman Abeid, Simiyu
CH A M A c h a Wa
f a n y a k a z i wa Serikali Kuu na Afya nchini (TUGHE) kimetishia kuwashtaki
waajiri wote wanaozuia kufanyika kwa vikao vya mabaraza ya wafanyakazi sehemu
za kazi yaliyoundwa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Kusudio hilo
limetolewa mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa, Ally Kiwenge
alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama hicho katika Mikoa ya Shinyanga na
Simiyu katika ziara yake ya mikoa ya Kanda ya Ziwa kuwahamasisha wafanyakazi
kufanya kazi kwa bidii.
Kiwenge alisema
pamoja na mabaraza ya wafanyakazi kuundwa kwa mujibu wa sheria, lakini bado
kuna baadhi ya waajiri ambao huzuia kufanyika kwa vikao vya mabaraza hayo na
kwamba kitendo hicho ni kupingana na sheria za uanzishwaji wake.
"Mabaraza
ya wafanyakazi yapo kwa mujibu wa sheria, wapo waajiri wanazuia yasifanyike na
wengine wanakataza yasiundwe, s a s a n iwa e l e z e wa z i kwamba TUGHE
tumeanza ufuatiliaji, mwajiri yeyote atakayebainika kuzuia vikao hivi kwa
makusudi hatutasita kumshtaki, tutampeleka mahakamani.
"Wapo
waajiri wanaodai kutopewa mafungu kwa ajili ya kuendeshea mabaraza hayo, sasa
tunaiomba Serikali ihakikishe inatoa fedha kwa ajili ya vikao hivyo, na
ninawaagiza makatibu wote wa TUGHE wa mikoa watoe taarifa za mwajiri ye yote
atakayetajwa kuzuia kufanyika kwa v i k a o h i v y o k a t i k a sehemu zao za
kazi, halafu waonetutakachokifanya," alisema Kiwenge.
Kwa upande mwingine k a t i b u m k u u
h u y o a l i w a t a h a d h a r i s h a viongozi wa vyama huru vya
wafanyakazi nchini k u t o k u b a l i k uwe kwa mifukoni na waajiri na kueleza
kuwa vyama hivyo vimeundwa kwa mujibu wa sheria, hivyo wahakikishe wanatimiza
wajibu wao katika kuwatumikia wanachama wao.
"Viongozi wa vyama vya wafanyakazi
tuwe makini tusikubali kugawanywa na waajiri, wapo ambao hivi sasa wanadiriki
kuwachagulia wafanyakazi wao vyama gani wajiunge navyo, hii ni hatari, tuache
kugombania wanachama, kila chama kishughulike na wanachama wake kwa mujibu wa
katiba yake," alisema Kiwenge.
No comments:
Post a Comment