Na John Gagarini, Kibaha
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoa wa
Pwa n i imemh u k umu mkazi wa Miembe Saba wilayani Kibaha, Amosi Chacha (40)
kwenda jela miaka 6 baada ya kukutwa na hatia ya wizi wa vocha za mtandao wa
simu pamoja na kukutwa na mihuri bandia.Mtuhumiwa
huyo alikutwa na hatia kwa makosa yote mawili yaliyokuwa yakimkabili katika
kesi iliyokuwa ikisikilizwa na Hakimu Mkazi, Aziza Mbadyo.
Mwendesha mashtaka wa
Serikali, Emmanuel Maleko ameieleza mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa akiwa
na mihuri ya Ofisa Mtendaji Mtaa wa Kwesimu pamoja na wa Kituo cha Ukaguzi wa
Maliasili cha Soni kilichopo Wilaya ya Lushoto Mkoa wa Tanga mnamo Juni 3, 2013
eneo la Sinza, Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam.
Imeelezwa kuwa
mtuhumiwa huyo alikuwa akitumia mihuri hiyo katika usafirishaji wa mali asili kutoka Tanga kwenda Dar es Salaam kwa lengo la kuweza kuvuka
vizuizi vya maliasili vilivyopo kwenye barabara kuu.Aidha Maleko
alieeleza mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa eneo la Kibaha Mkoa wa Pwani
akiwa na vocha za muda wa hewani zenye thamani ya sh. milioni 5 akizisafirisha
kwenda Tanga akitokea Dar es Salaam. Mwendesha Mashtaka
huyo wa Serikali aliongeza kuwa makosa yote hayo mawili alikutwa na hatia dhidi
yake, Chacha anadaiwa kuyatenda kwa nyakati tofauti.
Akisoma hukumu hiyo kwa muda wa saa moja na nusu, Mbadyo alisema kuwa
Mahakama imeridhika na maelezo ya upande wa Jamhuri hivyo imemtia hatiani Amosi
Mwita Chacha kwenda jela miaka sita ambapo katika kosa la wizi wa vocha alihukumiwa miaka minne na kosa la kukutwa na mihuri bandia alihukumiwa miaka
miwili hivyo adhabu zote mbili zitakwenda pamoja na atatakiwa kwenda Jela miaka
sita.
No comments:
Post a Comment