Rachael
Balama na Heri Shaban
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),
leo inatarajia kuwaburuta mahakamani baadhi ya vigogo wa mashirika ya umma
kujibu mashtaka yanayowakabili.
Vigogo hao walikuwa
wafikishwe kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijni Dar es Salaam jana,
lakini kutokana na baadhi ya taratibu kutokamilika watafikishwa mahakamani hapo
leo asubuhi.
Mmoja wa maofisa wa TAKUKURU aliyezungumza na Majira
kwa sharti la jina lake kutochapishwa gazetini, alithibitisha taarifa za
vigogo hao kuburutwa mahakamani leo
.
Hata hivyo, ofisa huyo alikataa kutaja majina na
mashirika waliyokuwa wakifanyia kazi vigogo hao. Jana maofisa wa TAKUKURU
walionekana mahakamani hapo wakihaha kukamilisha taratibu za kufikisha vigogo
hao mahakamani, lakini
Dkt. Edward Hosea ilishindikana
baada ya taratibu hizo kutokamilika.
Mmo j a wa ma o f i s a wa TAKUKURU
aliyezungumza na gazeti hili jana mchana, alisema imeshindikana kuwafikisha
mahakamani hapo jana na taratibu hizo zitaendelea leo.
Mmoja wa mawakili wa Serikali
aliyezungumza na gazeti hili, alithibitisha kesi za vigogo hao kusajiliwa
mahakamani hapo, lakini alikataa kutaja kesi hizo zinahusu watu gani na badala
yake aliwaelekeza waandishi wa habari kwenda kuuliza ofisi za makarani.
Mmoja wa makarani alipoulizwa alijibu;
"Nyie ni waandishi wa 10 kufika kuulizia suala hilo, lakini sina taarifa
hizo, wakifikishwa mtawaona.
No comments:
Post a Comment