Na Daud Magesa, Mwanza
WATU wasiofahamika
idadi yao wanaodhaniwa wezi,wameiba vielelezo katika stoo ndogo ya Kituo Kikuu
cha Polisi Kati, Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza baada ya kuvunja madirisha.Tukio la wizi huo
lilifanyika Julai 15, mwaka huu, majira ya usiku wa kuamkia Jumatano katika
jengo la Polisi Wilaya ya Nyamagana.Akizungumza na gazeti
hili jana, Kamanda wa Polisi Mkoa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ernest Mangu,
alisema wezi hao kabla ya kuingia ndani ya jengo hilo ,walivunja dirisha la
ofisi za Elimu, Ukaguzi Kanda ya Ziwa.
Alisema baada ya
kufanikiwa kuingia ndani ya ofisi hizo, hakuna walichoiba ndipo walivunja
dirisha na kuingia kwenye ofisi za Polisi Nyamagana.Alisema walivunja
dirisha na kutanua nondo kwa jeki na kisha kuingia kwenye stoo hiyo ndogo ambamo
vielelezo hivyo vilitunzwa.
Aliongeza kuwa baada
ya kuingia ndani ya stoo hiyo waliiba begi moja la nguo na kompyuta mbili
mpakato,moja ya kompyuta hizo ni kielelezo katika kesi ya ujambazi ambayo
mtuhumiwa alikamatwa nayo, ambaye kwa sasa yuko mahabusu katika Gereza Kuu la
Butimba.Kamanda Mangu alisema
kompyuta ya pili ni kielelezo cha kesi ya uharibifu wa mali inayomkabili fundi
mmoja na begi la nguo ambazo mwenyewe nazo hafahamiki.Alisema liliokotwa na
polisi baada ya kuwakurupusha wezi ambao walikimbia na kulitelekeza.
Alieleza kuwa eneo
walikopitia wezi hao usalama wake ni mdogo kwani ni uchochoroni na hakuna
ulinzi wala mwanga wa taa, hivyo wanajaribu kuangalia nani mmiliki wake kama
litakuwa ni mali ya taasis
i za serikali basi liendelezwe ili kuboresha usalama wa hapo na maeneo
jirani.
No comments:
Post a Comment