MBUNGE wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Bw. Stephen Ngonyani "Marufu
Profesa Maji Marefu" amesema wakala wa umeme vijijini (REA) tayari
wameanza utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati hiyo katika vijiji
mbalimbali vya wilaya hiyo.
Maji
Marefu aliyasema hayo juzi alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha
Makweli Kata ya Vugiri huku akivitaja vijiji ambavyo REA watafikisha umeme kuwa
ni Mkwakwani, Kwamzindawa na Gereza vilivyopo Kata ya Mnyuzi na Matalawanda,
Kijango, Mbuyu huko katika Kata ya Magoma.
Mbunge
huyo alivitaja vijiji vingine vitakavyofikiwa kuwa ni Makumba, Lusanga,
Kibaoni, Kijungu Moto, Dindira, Vugiri, Darajani, Mgobe, Makumba, Kituo cha
Afya Kwalukonge, Kitivo na kwenye miradi ya skimu za uwagiliaji Mombo,Kijango
na Kwamazandu utekelezaji wake utafanyika katika mwaka huu wa fedha 2013/14.
Maji
Marefu alisema upatikanaji wa miradi hiyo umetokana na ushawishi wake kwa bunge
na viongozi wenzake kuisukuma Serikali ili kufikisha huduma hiyo kwa wananchi
na kuweza kuharakisha maendeleo yao ambapo aliwasihi kuendelea kumpatia
ushirikiano kwa lengo la kutatua kero zinazowakabili.
"Ndugu zangu
ninachotaka kusema maendeleo siwezi kuyaleta peke yangu, ni ushirikiano kati
yangu mimi na ninyi wananchi kwa ushirikiano mlionipa nimebanana na wenzangu
bungeni hadi Serikali kupitia REA baadhi ya vijiji sasa vinapata umeme,"
alisema.
Akizungumzia utekelezaji wa
miradi hiyo ya umeme ya REA, Maji Marefu alisema kwamba, utekelezaji wake
tayari umeshaanza kwenye maeneo ya Magoma Mbuyu ambapo aliwaasa baadhi ya
watendaji kutojihusisha na masuala ya kisiasa badala yake watekeleze majukumu
yao kulingana na sheria na taratibu lengo likiwa kuharakisha upatikanaji wa
maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.
Wakati mbunge huyo
akiwasisitiza watendaji umuhimu wa kuzingatia kanuni na sheria katika utendaji
wao tayari kumeibuka suala la watendaji wa halmashauri kukwamisha ujenzi wa
madaraja katika tarafa ya Bungu ambapo licha ya mfuko wa jimbo kutolewa na
baadhi ya vifaa kununuliwa kazi hazifanyiki.
Hayo yalibainika kwenye
ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Mrisho Gambo na mbunge huyo walipotembelea
eneo hilo ambapo wananchi
walimlalamikia DC kuhusu kutotekelezwa kwa ujenzi wa madaraja ambapo kiongozi
huyo
wa serikali alilazimika kuwasiliana na mkurugenz kulikoni
No comments:
Post a Comment