JESHI la
Ulinzi la Wananchi w a Ta n z a n i a ( JWT Z ) linaadhimisha siku ya mashujaa
kila ifikapo Julai 25 ikiwa ni sehemu ya kuwakumbuka mashujaa waliopigana na
kushinda vita ya Kagera mwaka 1978/1979.Maadhimisho hayo hufanyika
mara moja kwa mwaka na mwaka huu yanafanyika leo katika Mkoa wa Kagera Wilaya
ya Bukoba kwenye makaburi ya mashujaa yaliyopo Kaboya.
Mgeni rasmi katika
maadhimisho hayo atakuwa Rais wa Jamhuri ya muungani wa Tanzania na
Amiri Jeshi Mkuu Dkt.Jakaya Kikwete ambapo watakuwepo viongozi waandamizi wa
Serikali, vyombo vya Ulinzi na Usalama, vyama vya siasa, taasisi za dini na
taasisi mbalimbali za kiraia.
Maombolezo ya uwekaji wa
silaha za asili, usomaji dua kutoka kwa viongozi wa madhehebu mbalimbali ya
dini.
Wachache wanaowafahamu
majina ya mashujaa wetu ambao tunawaheshimu lakini wengi wao hawayafahamu kwa
majina ila tunafahamu tu ya kwamba walipigana na kufa, katika jitihada za
kutetea uhuru wa nchi yetu.Tunawakumbuka na kuwaheshimu.
Leo tunawakumbuka mashujaa
hao kwa fahari. Juhudi zao na vitendo vyao vilivyotutia moyo siku za nyuma na
vinatutia moyo mpaka sasa. Ni vizuri Taifa likaendelea
kuwaenzi mashujaa hao kwa namna ya kipekee kwani hata kwa kuwatangaza majina yao ili waweze kufahamika
kwa si wa kizazi hiki hata cha baadaye.
Hali ya amani na utulivu wa
nchi yetu umekuwa si wa kuridhisha hivyo kama mashujaa hao wangeeleza namna
ambavyo ilivyokuwa katika mapigano na watu walivyokufa nina imani kuwa
ingesaidia kupunguza viashiria vya uchochezi wa vita kwa baadhi ya watu wenye
mlengo wa kuwania jambo fulani.
Katika kuhakikisha kuwa
mashujaa hao wanakumbukwa, Mkoa wa Kagera umepewa heshima kubwa ya kuandaa
maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa kitaifa mwaka 2013 ambayo
yanaadhimishwa leo katika Wilaya ya Muleba katika Kambi ya Jeshi la Wananchi
Kaboya.
Kanali Mstaafu Fabian
Massawe ambaye ni Mkuu wa Mkoa anasema kuwa maadhimisho hayo yataambatana na
ziara ya kikazi ya Rais Jakaya Kikwete katika mkoa huo.
Anasema kuwa kamati
zilizopewa jukumu la kuandaa maadhimisho ni Kamati ya Mapokezi, Usafiri na
Malazi, Kamati ya Ujenzi Uwanja na Mapambo, Kamati ya Chakula na Afya, Kamati
ya Ulinzi na Usalama na Kamati ya Burudani, Habari na Uhamasishaji ambazo zote
zimefanikiwa kumaliza kazi zake.
"Maandalizi yote yamekamilika
na tumepokea wageni kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya mkoa, pia nje ya
nchi watakaohudhuria maadhimisho hayo," anasema.
Anasema kuwa ni vizuri
wananchi wa mkoa huo wakawa wakarimu kwa wageni wote watakaofika kwa kutekeleza
majukumu kama Wanakagera .
Kati ya mambo ambayo
wananchi wanatakiwa kuyazingatia ni kila mwananchi kuhakikisha maeneo yake na
mazingira yanayomzunguka yanaendelea kuwa katika hali ya usafi kama utamaduni wetu. Pia kumwajibisha mtu yeyote
atakayeonekana anachafua mazingira yetu.
Anasema kuwa kila mwananchi
anatakiwa kushiriki kikamilifu katika kuadhimisha siku yenyewe ya Kumbukumbu ya
Mashujaa katika eneo la Kaboya.
"Hatuna budi
kuwakumbuka Mashujaa wetu kwa sababu ya historia ya mkoa wetu kushiriki katika
vita ya kumwondoa adui aliyekuwa amevamia nchi yetu kupitia ardhi ya mkoa huu
mwaka 1978 hadi 1979," anasema kanali Massawe.
Anasema kuwa ni jukumu la
kila mwananchi kuhakikisha anaitunza amani na utulivu kama
destuli ya mkoa huo na taifa kwa ujumla ili kuendelea kuwaenzi mashujaa kwa
amani na utulivu.
Katika kuhakikisha kuwa
sikukuu hiyo inaadhimishwa kwa amani na usalama, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya
Mkoa imejipanga vizuri kuhakikisha amani na utulivu vinatawala wakati wote.
"Kwa mwananchi yeyote atakayeona viashiria vya
uvunjifu wa amani atoe taarifa mara moja ili taarifa hizo zifanyiwe kazi mara
moja,' anasema.
Anasema katika maadhimisho hayo Mkoa wa Kagera
umepokea wageni 1,500 wakiwemo mabalozi wanaowakilisha nchi mbalimbali pamoja
na wageni wengine toka nje ya nchi.
Anasema kuwa Rais Kikwete anatarajia kufanya ziara
ya kikazi katika mkoa huo ambapo anatarajia kuzindua miradi mbalimbali ya
maendeleo kama kuweka jiwe la msingi katika
ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.
Pia anatarajia kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa
barabara ya kiwango cha lami ya Kagoma- Rusahunga, kuweka jiwe la msingi
barabara ya kiwango cha lami Kyaka hadi Bugene,kufungua Jengo la Mahakama Kuu
Kanda ya Bukoba.
Kanali Massawe anasema kuwa pia rais anatarajia
kufungua jengo la kitega uchumi la Chama Kikuu cha Ushirika (KCU Ltd), kuzindua
mradi wa maji Muleba, kuzindua kivuko kipya Rusumo (Ngara), kuzindua mradi wa
usambazaji umeme vijijini Nyaishozi (Karagwe), kuzindua Wilaya Mpya ya Kyerwa
"Pia rais atazungumza na wananchi kupitia
mikutano mbalimbali ya hadhara katika wilaya zetu ndani ya mkoa ninawaomba
wananchi mjitokeze kwa wingi kumsikiliza," anasema.
No comments:
Post a Comment