17 July 2013

TANAPA YATOA MSAAA WA MABATI 6,000


Na Timothy Itembe, Tarime
SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia Hifadhi ya Wanyama Serengeti imetoa msaada wa mabati 6,000 katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara kama sehemu yao ya kutekeleza miradi ya maendeleo katika Wilaya na vijiji vinavyozunguka Hifadhi za Taifa.
Akikabidhi mabati hayo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, John Tuppa, Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi za Taifa, Allan Kijazi amesema kuwa Tanapalimetoa mabati 6,000 yenye thamani ya sh.milioni 124 kwa ajili ya kusaidia katika maendeleo ya wananchi.

Kijazi amesema kuwa mabati hayo yatasaidia kuezeka madarasa ya shule, nyumba za walimu na vituo vya polisi na zahanati ndani ya Wilaya ya Tarime na kwamba msaada huo unatokana na ushirikiano na mahusiano mazuri kati ya Tanapana Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.
Akielezea changamoto Kijazi alisema kuwa kumekuwepo na migogoro baina ya wananchi na Hifadhi ya Serengeti kwa kujenga nyumba katika maeneo ya hifadhi na kuchunga mifugo hifadhini, kuchoma mkaa, huku baadhi ya wananchi wakiwaua wanyama kwa ajili ya vitoweo jambo ambalo amedai kuwa linavunja mahusiano mazuri baina yao na wananchi katika maeneo yaliyo jirani na hifadhi.
Kijazi aliongeza kuwa changamoto nyingine kumekuwepo na baadhi ya viongozi wa kisiasa kutetea uovu na kushawishi wananchi kuendelea kuchunga mifugo katika maeneo ya hifadhi na hivyo kusababisha mkanganyiko kati ya wananchi na hifadhi.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara John Tuppa amewataka viongozi wa kata na vijiji kutohusisha siasa katika maendeleo ya wananchi na badala yake watatue matatizo ya wananchi ili kuwepo na mahusiano mazuri kati yao na Shirika la Tanapa.
Tuppa amewataka wananchi kutojihusisha na vitendo vya kuua wanyama kwakuwa wanyama ni vivutio vya watalii na kupitia wanyama hao taifa linapata fedha ambazo zinatumika katika maendeleo ya wananchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele amelishukuru Shirika la Tanapakwa msaada wa mabati akawataka wananchi kulinda mapitio ya wanyama kwa madai kuwa wanyama wanatoka nchi jirani ya Kenya kuingia Hifadhi ya Serengeti

No comments:

Post a Comment