Na Darlin Said
TAASISI za fedha nchini zimetakiwa kuwa na utaratibu u t a k a o r a h i
s i s h a upatikanaji wa huduma zaidi za kifedha kwa wananchi wanaoishi
vijijini ili kufikia maendeleo endelevu.
Mwito huo ulitolewa jijini Dar es Salaam na Mtafiti Mwandamizi wa
Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Uchumi na Jamii (ESRF), Dkt. Donatilla Kaino,
wakati wa kongamano lililolenga kutoa taarifa juu ya matokeo ya utafiti wa hali
halisi ya upatikanaji wa huduma za kifedha katika sekta ya kilimo au AgFiMS
Tanzania 2011 Demand Side Technical Report kwa maofisa wa wizara.
Alisema upatikanaji haraka na rahisi wa huduma za fedha kwa wananchi
vijijini ni muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Alifafanua kwamba wakazi vijijini ambao shughuli yao kubwa ni kilimo
ndiyo wengi zaidi nchini na hivyo litakuwa ni jambo la busara kama taasisi za
kifedha zitafikiria kuimarisha huduma zao katika maeneo hayo ili kufikia
maendeleo ya kweli.
Alisema
huu ni wakati mwafaka kwa watu kujenga tabia ya kujiwekea akiba kama kweli wanataka
maendeleo.
"Kujiwekea akiba ni muhimu kwa mtu binafsi, jamii na taifa zima...
tunatakiwa kujenga tabia hii kwa watoto mapema iwezekanavyo," alisema.
Awali akifungua mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa ESRF, Dkt. Bohela
Lunogelo, alisema nafasi ya sekta ya fedha ni muhimu kwa sasa kuliko kipindi
chochote katika historia ya Tanzania.
Madhumuni ya ripoti ya AgFiMS Tanzania 2011 ni kusaidia maendeleo ya
huduma za fedha kuchochea biashara katika kilimo na kufikisha huduma hizo kwa
wakulima.
Kwa mujibu wa wataalamu, maendeleo ya
kilimo ni njia bora ya kupunguza umaskini. Asilimia 75 ya watu maskini katika
nchi zinazoendelea wanaishi vijijini na asilimia 85 ya watu hao wanategemea
kilimo kuendesha maisha yao.
No comments:
Post a Comment