Na Martha Fataely, Moshi
WATU sita
wanashikiliwa na Polisi mkoani Kilimanjaro na Arusha wakiwemo raia wawili wa
Kenya kwa tuhuma za kukutwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya mlima Kilimanjaro
(KINAPA) bila kuwa na kibali.
Miongoni mwa
watu hao sita watuhumiwa wanne walikamatwa jijini Arusha, watatu wakiwa wa
familia moja kwa kukutwa na nyara mbalimbali za Serikali na mmoja kwa kukutwa
na silaha inayodaiwa kutumika kwenye ujangili.
Akizungumzia
tukio la waliokatwa KINAPA, Meneja Uhusiano TANAPA, Pascal Shelutete alisema
watu wawili walikamatwa juzi katika njia ya Marangu eneo la Mandara wakizunguka
katika eneo la msitu wa hifadhi hiyo.
Aliwataja raia
wa Kenya waliokamatwa ni Robert Mwadime Mwakana (30) na Dickson Kawa Mbole
(27), wote wakazi wa Taveta nchini Kenya waliodaiwa kutumia njia zisizofahamika
kuingia hifadhini humo.
Kwa watuhumiwa wa familia moja, waliokamatwa
jijini Arusha na nyara za Serikali, Shelutete aliwataja kuwa ni Charles Mollel,
Alex Mollel na Samwel Mollel ambao walikutwa eneo la Kisongo Olasite jijini
humo.
Shelutete alisema watuhumiwa hao wa
familia moja walikamatwa kwa tuhuma za kukutwa na nyara za Serikali ambazo ni
mifupa mitatu ya twiga yenye uzito wa kilo 10.4 na mfupa mmoja wa tembo wenye
uzito wa kilo tano.
Aidha alisema Hifadhi ya Taifa Arusha kwa
kushirikiana na Polisi mkoani humo walimkamata mtuhumiwa mwingine mmoja Elias
Sifael mkazi wa Leguruki Nkoasenga kwa kukutwa na silaha aina ya shotgun namba
C 139415 inayoaminika kutumika kwa ujangili.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoani
Kilimanjaro, Robert Boaz alisema yupo nje ya ofisi na kuwataka waandishi wa
habari kusubiri mpaka atakapokuwa ofisini ili kutolea taarifa tukio hilo
No comments:
Post a Comment