16 July 2013

SIMBA YATUA MUSOMA KUHITIMISHA ZIARA YAO


 Shufaa Lyimo na Nasra Kitana
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wametua mjini Mu s oma Mk o a wa Mara jana katika ziara yao ya kimichezo ambapo kesho watacheza na Kombaini ya huko.
Katika mechi yake ya kirafiki iliyochezwa juzi mjini Kahama Simba waliifunga timu ya Kahama United bao 1-0, bao hilo lilifungwa na Zahor Pazi mchezaji mpya wa Simba.

Akizungumza kwa simu jana wakiwa njiani kuelekea Musoma Kocha Mkuu wa timu hiyo Abdalla Kibadeni alisema, mara baada ya kufika mjini humo watacheza mechi na Kombaini ya huko au timu yoyote watakayoandaliwa.
"Sasa hivi tupo njiani tunaelekea Musoma tumetoka alfajiri lakini mpaka sasa bado sijajua tutakutana na timu gani ingawa tumepanga kucheza na kombaini ya huko ila tukifika tutajua,"alisema Kibadeni.
Alisema kikosi chake kwa sasa kinaendelea vizuri na kila mchezaji ana morali wa hali ya juu kuhakikisha msimu ujao wanafanya vizuri.
"Kikosi changu kinaendelea vizuri kabisa na vijana wote wapo katika hali nzuri wakiwa na imani ya kufanya vizuri msimu ujao wa ligi kuu ambao utaanza mwezi ujao," alisema,
Simba iliondoka wiki iliyopita ambapo mchezo wake wa kwanza ilikutana na timu ya Rhino Rangers na kuwafunga mabao 3-1, wakati mchezo wa pili ilicheza na Kahama Utined na kuifunga bao 1-0.
Wakati huo huo Kaimu Mwenyekiti wa Simba Joseph Itang'are amesema kuwa timu yao ipo fiti kuivaa URA ya Uganda watakayochezanayo Julai 20, mwaka huu.
"Kiukweli timu yetu sasa inaleta raha kwakuwa kila mechi vijana wanafanya vyema na tunaahidi hata tukicheza na URA pia lazima tuwapige bao," alisema Itang'are.

No comments:

Post a Comment