18 July 2013

SERIKALI YASHAURIWA KUONGEZA BAJETI YA MAJI


 SERIKALI imeshauriwa kutenga bajeti maalumu kwa ajili ya kusaidia kuendeleza miradi ya maji ili wananchi waweze kuepukana na adha ya kutembea umbali mrefu kusaka huduma hiyo, anaripoti Lilian Justice, Morogoro.
Ushauri huo ulitolewa jana mkoani Morogoro na Diwani wa Kata ya Bigwa, Zamoyoni Abdalah wakati akizungumza na majira ofisini kwake.
Abdalah alisema kuwa kutokana na wananchi kukumbana na kero kubwa ya ukosefu wa maji katika maeneo mengi kumepelekea kushindwa kushiriki kikamilifu katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

“Serikali vyema ikatenga bajeti maalumu ya kutosheleza kuendeleza miradi ya maji kuanzia ngazi ya chini kwani ndiko kuliko na changamoto kubwa,” alisema .
Aidha Diwani huyo alisema kuwa katika kukabiliana na changamoto hiyo tayari kwenye kata yake kumeanzishwa mradi wa I-WASH ambao umesaidia kujenga tenki kubwa la maji ili kuweza kuwasaidia wananchi kupata huduma hiyo kwa urahisi ukilinganisha na hapo awali.
"Mradi huu wa I-WASH wa kutoka nje umeweza kujenga tenki lililogharimu kiasi cha shilingi mil.78 na unahudumia katika Kata ya Bigwa ambapo umeweza kuwahudumia wananchi wapatao 2,800.
Aidha alitoa wito kwa wananchi kuepuka kuharibu miundombinu ya miradi mbalimbali inayoanzishwa ndani ya kata hiyo ikiwemo ya maji kwani kutapelekea kukosa huduma muhimu sambamba na wahisani kushindwa kuwasaidia katika masuala mbalimbali ikiwemo ya kiuchumi afya na hata barabara.
“Tunaomba kila mwananchi awe mstari wa mbele kulinda miundombinu na atakayebainika k u j i h u s i s h a n a u h a r i b i f u atachukuliwa hatua kali za kisheria kwani miundombinu iliyopo au inayoanzishwa ni mali ya wananchi hivyo haina budi kutunzwa ili iweze kuwa endelevu kwa kizazi hadi kizazi,” aliongeza.

No comments:

Post a Comment