Na Rehema Mohamed
WADAU
wa elimu nchini, wamesikitishwa na kitendo cha kushindwa kujazwa kwa nafasi
10,074 za kidato cha tano kutokana na kufeli mtihani kwa wanafunzi waliomaliza
kidato cha nne 2012 na kuitaka Serikali itekeleza kwa vitendo ushauri ambao
wameutoa ili kuinua kiwango cha elimu nchini.
Ushauri huo ulitolewa Dar es Salaam jana kwa
nyakati tofauti na wadau hao akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu, Bi.
Elizaberth Missokia, ambaye alisema Serikali inapaswa kuwa na mfumo mzuri wa
kuandaa walimu wenye sifa badala ya kupeleka vyuoni wale
waliofeli.
"Mazingira
ya shule yanapaswa kuwa ya kuridhisha, vifaa viwepo ili msingi wa kufundisha
uwe imara, wanafunzi wasibebeshwe masomo mengi ambayo hayana faida,"
alisema Bi. Missokia.
Al i s ema u p
o umu h imu wa walimu kupatiwa mafunzo wakiwa kazini na mitaala
inapobadilishwa, washirikishwe na kupewa mafunzo ambapo ruzuku iliyotengwa ili
kupelekwa shuleni, iwafikie wahusika kwa wakati ili kuwawezesha walimu wanunue
vitendea kazi.
"Madai ya
walimu yapatiwe ufumbuzi kwani wasipokuwa na kipato cha kutosha ni vigumu kuwa
na ari ya kufanya kazi na wale wanaofanyakazi katika mazingira magumu wapewe
motisha ili waweze kujituma zaidi," alisema.
Aliwataka Watanzania wasimame imara
kuhakikisha watoto wao wanapata elimu bora ambayo ni haki yao kikatiba ambapo
mwanafunzi anapokosa msingi mzuri kuanzia ngazi ya chini ni athari kwake hasa
anapofika Chuo Kikuu.
Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Ardhi, Profesa
Alphonce Kyessi, alipoulizwa uzoefu aliopata kwa wanafunzi wa sasa
ukilinganisha na kipindi cha nyuma, alisema vijana wengi vyuoni hawataki kwenda
maktaba kujisomea wanafunzi
wengi hawasomi kabisa tofauti na zamani, ukishafundisha baadhi yao hawaendi
maktaba kusoma na wengine usipokuwa makini hata notisi hawachukui kabisa,"
alisema.
Alisema idadi ya wanafunzi mashuleni
ni kubwa ukilinganisha na nyenzo zilizopo tofauti na zamani ambapo mfumo wa
elimu ulikuwa sio mbaya bali nyenzo ndiyo hazipo kabisa.
Naye Profesa Ngemba Maruku kutoka
Chuo Kikuu cha Mzumbe, alisema kuwa viwango vya elimu vimepungua kwa sababu
walimu wamekosa mori wa kufundisha na baadhi yao hawasomi kwa nia ya kujifunza
bali wanataka kumaliza masomo.
Aliitaka Serikali ikubali kutumia
fedha za kutosha kuwekeza katika sekta ya elimu ili kuleta mabadiliko kwa
kuajiri walimu, kuboresha mazingira ya kazi na ufundishaji.
No comments:
Post a Comment