Na Mwandishi Wetu
BENKI ya Taifa
ya Biashara (NBC), imezindua Kampeni ya Uelewa ya Mikopo kwa Makundi, huduma
itakayowalenga waajiriwa wenye mishahara.
NBC ni moja
kati ya benki zenye kuaminika nchini ikiwa na uzoefu wa zaidi ya miaka 45
katika kutoa huduma za kifedha.
Aidha, mpango
huo wa mikopo kutoka NBC unalenga kuwanufaisha waajiriwa wanaopata mishahara
huku wakibanwa kwa kutokuwa na kipato cha ziada kinachoweza kuelekezwa ama
kwenye uwekezaji au shughuli nyingine yoyote.
Sharti pekee
linalomfanya mwajiriwa kukubalika kwenye mpango huo ili kupata mkopo ni
uthibitisho kutoka kwa mwajiri wake
.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo ya uelewa iliyofanyika Makao Makuu ya NBC
jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo Mizinga Melu
alisema hayo ni mafanikio.
"Hii ni
hatua muhimu sana kwa benki yetu, kwa kufanikiwa kutimiza moja ya malengo yetu
ya kuwasaidia watu kufikia matamanio yao, kwa njia sahihi. Tunaishi kwenye
mazingira magumu ya kiuchumi ambapo kipato cha wengi kinashindwa kukidhi
mahitaji yao.
“Kwa hiyo, kwa
kupitia mpango huu tutasaidia kuwapunguzia wateja wetu mzigo mkubwa walionao
kwa kuwapa fursa ya kufanya mengi zaidi kutokana na fedha zao," alisema.
Alisema, mikopo
ya NBC kwa makundi ipo katika aina mbili ikiwemo ya Mfumo wa Mikopo ya
Uthibitisho (NBC Group Loan Guarantee Scheme) ambayo mwajiri anakuwa
mthibitishaji mkuu kwa mikopo ya waajiriwa (wafanyakazi) wake.
Pia alisema
kuna Mikopo ya NBC kwa Makundi (NBC Group Loans Scheme) ambapo mwajiri anasaini
Mkataba wa Makubaliano (MoU) n a k u t a k iwa kuleta benki mishahara ya
mwajiriwa pamoja na madai mengine.
"Ukifananisha
na mipango mingine ya mikopo, huu wa NBC umetengenezwa kwa kuendana na mfumo wa
maisha wa wateja wetu. Ulipaji wake ni rahisi kwani unaendana vyema na wakati,
muda na kiwango cha malipo ambacho ni kidogo na kila mmoja anakimudu,” alisema
Melu.
Hata hivyo, kiwango cha chini kabisa cha
mikopo hiyo ni sh. 1,000,000 na cha juu ni sh. milioni 50 katika kipindi cha
malipo cha kati ya miezi sita hadi 60 (miaka mitano).
"Ninawashauri waajiri n a w a a j i r
i w a w o t e kuitumia ipasavyo nafasi hii kutoka NBC. Mpango huu utawanufaisha
sana waajiriwa kwani hawana haja ya kuwa na dhamana binafsi ili wanufaike nao.
Dhamana pekee ni ajira yao.
" L i k i t o k e a j a m b
o lisilotarajiwa kama kifo au ulemavu wa kudumu, h a k u t a k uwa n a d e n i
litakalobaki kwa wategemezi wa mkopaji kwani bima ya mkopo italitatua hilo,”
alisisitiza Mkurugenzi huyo.
punguzeni riba kwanza ndio mtuzindulie hiyo kampeni!
ReplyDelete