18 July 2013

MWEI YAWEZESHA WANAWAKE 400


 Na Mwandishi Wetu
WANAWAKE 400 k a t i k a Wi l a y a y a T e m e k e wamenufaika na mikopo isiyokuwa na riba, hii ni katika utekelezaji wake wa azma ya kampuni ya mawasiliano ya Vodacom kubadili maisha ya wanawake kwa kuwawezesha kukuza mitaji ya biashara na kuongeza kipato.
Meneja wa mpango huo kusaidia wanawake wanaojishughulisha na biashara ndogondogo (MWEI), Grace Lyon alisema hayo juzi jijini Dar es Salaam wakati wa mchakato wa kuwapatia mikopo nafuu isiyo na riba wala dhamana. Alisema kuwa, kampuni hiyo imepanua wigo wa mpango wake ambapo sasa inawafikia wanawake hata wa mijini.

Alisema kuwa wanawake wajasiriamali zaidi ya 400 wamepatiwa mkopo huo ili kujiendeleza kiuchumi na kuwa na familia zenye maendeleo.
Alisema kuwa pamoja na kuwepo kwa maombi ya kuwafikia wanawake wa mijini kampuni ya Vodacom imekubaliana na mawazo hayo na kwamba wanawake wa mijini watajiweka tayari kutumia fursa ya mikopo ya Mweikujiinua kiuchumi.
“Kwa zaidi ya miaka minne sasa Mwei imekuwa ikielekeza nguvu zake vijijini ambako tayari tumewafikia wanawake wengi katika mikoa mbalimbali, sasa tumeona ni vyema mafanikio yale yawafikie na wanawake wa mijini ambao nao kimsingi wanahitaji kujengewa uwezo wa kumudu maisha,” alisema Lyon
Kuhusu utekelezaji wa azma hiyo, Lyon alisema wameanza na Temeke lakini mipango ni kuzifikia wilaya nyingine za jiji la Dar es Salaam huku akiwasihi wanawake hao kutambua kuwa hakuna kikubwa kilichoanza na kingi bali siku zote kikubwa huanza na kidogo.
Kwa upande wao baadhi ya wafanyabiashara hao wa Temeke wameelezea kufurahishwa na mpango huo hasa katika kipengele cha kutokuwepo kwa riba katika mikopo hiyo.

No comments:

Post a Comment