12 July 2013

MWANAFUNZI KORTINI KWA KUBAKA


 Na Abdallah Amiri, Igunga
JESHI la Polisi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora limemfikisha mahakamani Masanja Ndongo 15, Mkazi wa Igunga mjini kwa kosa la kubaka mtoto mwenye umri wa miaka mitatu.
Mshtakiwa huyo alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga jana saa 11:30 asubuhi huku wananchi wakiwa wamefurika mahakamani hapo kushuhudia kesi hiyo.
Akisomewa shtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Igunga, Ajali Milanzi, Mwendesha mashtaka wa Polisi, Dezidery Kaigwa alisema kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Julai tisa mwaka huu saa 12:00 jioni katika Mtaa wa Kilabu cha chini wilayani humo.
Aidha mwendesha mashtaka huyo alisema kuwa mshtakiwa huyo ni mwanafunzi anayesoma darasa la sita katika Shule ya Msingi Chipukizi iliyoko mjini Igunga.
Alisema kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 130(1)na 2(e)pamoja na kifungu namba 131 sura ya 16 ya kanuni ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Mshtakiwa baada ya kusomewa shtaka alikana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande baada ya kukosa mdhamini na kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 26, mwaka huu itakapotajwa tena

No comments:

Post a Comment