. LONDON, Uingereza
KOCHA Jose Mourinho amesema Wayne Rooney
ndiye shabaha pekee ya uhamisho majira ya joto kwa Chelsea
baada ya Manchester United kuikataa ofa yao
kumsaini mshambuliaji huyo wa England.
Mourinho alikanusha taarifa kwamba
David Luiz au Juan Mata walikuwa wabadilishane na Rooney.
Kocha huyo Mreno anatarajiwa kuzungumza
na waandishi wa habari kesho wakati Chelsea
watakapotua Malaysia katika
ziara yao kabla
ya msimu wa ligi kuanza.
Taarifa za Chelsea kumtaka mshambuliaji huyo zilivuja
siku ambayo makamu mwenyekiti wa United, Ed Woodward, aliporudi mapema kutoka
ziara ya klabu kabla ya msimu wa ligi kuanza.
Hata hivyo, Man United
imesisitiza kwamba kurudi kwa Woodward hakuhusiani na suala la Rooney.
No comments:
Post a Comment