- Ni wa JWTZ waliouwawa jimbo la Darfur, kusafirishwa kwa maziko
Na
Mwandishi Wetu
MIILI ya
askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ) waliouawa katika shambulio la kushtukiza katika Jimbo la Darfur, nchini Sudan itaagwa leo katika Viwanja vya Makao Makuu
ya Jeshi, Upanga, jijini Dar es Salaam
kuanzia saa 3 asubuhi na baadaye kusafirishwa kwenda kwao kwa ajili ya maziko.Habari
ambazo gazeti hili limepata, zimeeleza kuwa wanajeshi hao wataagwa kwa heshima
zote za kijeshi na mara baada ya hapo, miili hiyo itasafirishwa kwenda kwao kwa
ajili ya maziko. Wanajeshi waliouawa katika tukio
hilo wakiwa katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa (UN) mjini
Darfur ni Sajini Shaibu Shekhe, Koplo Osward Paul Chaula, Koplo Mohamed Ally,
Koplo Mohamed Chukilizo, Rodney Ndunguru, Fortunatus Msove na Peter Werema.
Miili ya wanajeshi hao iliwasili
nchini jana na kupokewa kwa vilio, simanzi na huzuni kutoka kwa ndugu, jamaa,
marafiki pamoja na viongozi wa kitaifa wakiongozwa na Makamu wa Rais, Dkt.
Mohamed Gharib Bilal.Ndege maalumu iliyobeba miili ya
askari hao yenye namba B 737-400 Comb ZS-JRQ iliwasili jana kwenye Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal One (Air Wing) saa 10.39.
A s k a r i h a o w a l i k u w a wakiwasindikiza waangalizi
wa amani kutoka Khor Abeche kwenda mjini Darfur.Inaelezwa kuwa shambulio hilo
lilitokea umbali wa kilomita 20 kutoka Makao Makuu ya kikosi hicho ambapo
miongoni mwa waliojeruhiwa ni pamoja na maofisa na askari kutoka mataifa
mengine.Wakati kikosi cha askari jeshi wa Tanzania
kikishambuliwa, kilikuwa na askari 36 ambao ni miongoni mwa askari wanaolinda
amani kwenye Kikosi cha UN mjini Darfur nchini Sudan
No comments:
Post a Comment