BARCELONA,
Hispania
BA R C E L O N A wamemchagua Gerardo
Martino kutoka Argentina kama kocha wao mpya baada ya kukubali mkataba wa miaka
miwili kuifundisha klabu hiyo.Martino (50), kocha wa zamani wa Paraguay, anachukua nafasi ya Tito Vilanova,
ambaye alijiuzulu kama kocha wa Barcelona
ili aendelee na matibabu yake ya saratani.
Martino hivi karibuni alikuwa
akiifundisha klabu ya Old Boys ya Newell, ambao aliwaongoza kunyakua kombe la Argentina la
Torneo msimu uliopita. Taarifa za kuwasili kwake Barcelona zilitarajiwa
kutangazwa jana na mabingwa hao wa Hispania.
Martino anakuwa raia wa nne wa Argentina
kuifundisha Barca baada ya Helenio Herrera, Roque Olsen na Cesar Luis Menotti.
Hiyo itakuwa kazi ya kwanza kwa Martino
nje ya Amerika ya Kusini tangu alipoichezea Tenerife
kwa miezi sita mwaka 1991.
Awali, makocha wengi walikuwa wakihusishwa
kutaka kujaza nafasi hiyo, akiwemo kocha Luis Enrique wa Barcelona B, Andre
Villas-Boas wa Tottenham, Michael Laudrup wa Swansea na Guus Hiddink, ambaye juzi alijiuzuru
kuifundisha Anzhi Makhachkala
No comments:
Post a Comment