BANGKOK,
Thailand
KLABU ya Manchester United, juzi asubuhi wametua jijini
Bangkok ikiwa ni kituo chao cha kwanza cha ziara yao ya kimataifa wakiwa na
kocha David Moyes, ambaye anapata uzoefu wake wa kwanza kwa mashabiki wa klabu
hiyo duniani kote.
Mabingwa hao wa Ligi Kuu England, watasafiri zaidi ya
maili 20,000 na kutua katika majiji matano ya nchi nne huku wakijiandaa na Ligi
Kuu kuwakabili majirani zao Man City na Chelsea ya Jose Mourinho.
Rio Ferdinand, anategemea United wataongeza makali
zaidi, kabla ya msimu kuanza kutokana na kutaka kumfurahisha Moyes.
"Ni ukweli kwamba kila mmoja anajaribu kufanya kweli
katika ziara hii," Ferdinand alisema katika tovuti ya klabu.
Kwa mujibu wa Daily Mail, Kocha Mkuu Moyes,
alipokelewa kwa kishindo na wale waliojitokeza kuipokea United kwenye uwanja wa
ndege na kwenye hoteli waliyofikia.
Kazi ya kwanza kwa Moyes, akiwa na Giggs, ambaye
amechukua jukumu la kuwa kocha mchezaji msimu huu, ilikuwa kusaini kitabu cha
salamu za kheri kwa Mfalme wa Thailand, anayeheshimiwa mno katika nchi hiyo.
Ingawa wachezaji wa United
waliruhusiwa kupumzika, mazoezi ya ndani yalipangwa kufanyika baadaye siku
hiyo.
No comments:
Post a Comment