Na Mwandishi Wetu, Mbeya
MASHINDANO ya kumsaka nyota wa kuimba wa
Epiq Bongo Star Search (EBSS), yamezoeleka kuwa na majaji watatu ambao ni Ritha
Paulsen, Salama Jabir na Master Jay, lakini kwa mara ya kwanza, vijana waliojitokeza
kwenye usaili mkoani Mbeya walipata fursa ya kusailiwa na majaji wapya wa
kutokea mkoani hapa.
Majaji hao,
Stanslaus Lambert na Fredy Mabula ambao waliongezwa ili kuleta ladha tofauti
kwenye mashindano hayo, wamepongeza EBSS kwa kusaidia vipaji vilivyoko mikoani.
"Epiq
Bongo Star Search ina mchango mkubwa mno kwenye tasnia ya muziki hapa nchini,
hivyo ni heshima ya pekee kuwa jaji kwenye mashindano haya," alisema
Mabula.
Wakizungumzia
uwezo wa majaji wapya, Master Jay alisema wameonesha uwezo katika kuwashauri
washiriki na kuchagua vipaji vinavyofaa.
Awali Jaji Mkuu
wa EBSS, Ritha alisema kuingia kwa majaji hao wapya ni mwendelezo wa utaratibu
walioanzisha sasa wa kushirikisha majaji kutoka mazingira, ambayo mchujo
unafanyika.
"Lengo
letu ni kuifanya EBSS imguse kila mtu, lakini pia ichague kila aina ya vipaji
vilivyopo mikoani na iviendeleze," alisema Ritha.
Akizungumzia
hali ilivyokuwa kwenye usaili wa mkoa huo, Ritha alisema washiriki wameonesha
uwezo mkubwa katika kuimba na kujiamini.
Jaji huyo
alisema Mkoa wa Mbeya ni mkoa ambao umewaridhisha majaji kati ya mikoa mitatu
ya Dodoma na Zanzibar, ambako wameshafanya usaili hadi sasa.
Mbeya imetoa washiriki sita ambao wamepata tiketi
ya kushiriki katika fainali zitakazofanyika Dar es Salaam, kwa sasa EBSS
inakwenda mkoani Mwanza wiki h
.
No comments:
Post a Comment