Na
Mosi Mrisho
MABONDIA 1
0 wa t imu y a Ta i f a y a ngumi, wanajiandaa na mashindano ya kuwania ubingwa
wa Afrika, ambayo yanatarajia kufanyika kuanzia Septemba Mosi hadi 7 mwaka huu
nchini Mauritius.Akizungumza na mwandishi wa
habari hizi Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa
Tanzania (BFT), Makore Mashaga alisema mabondia hao wameshaanza mazoezi katika
Uwanja wa Taifa wa ndani, Dar es Salaam.
"Mabondia
watakaoshiriki mashindano hayo hivi sasa wapo katika mazoezi chini ya makocha
watano na tunaamini kwa mazoezi hayo watafanya vizuri," alisema.Hata hivyo Mashaga alisema mabondia hao ni wachache
kulingana na mashindano hayo. Aliwataja
makocha hao kuwa ni Remmy Gambo, Edward Emmanuel, Mzonge Hassan, Benjamin
Mwagata na Mussa Mwaisori.
No comments:
Post a Comment