Ester
Maongezi na Neema Malley
MKURUGENZI wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred
Lwakatare, amewekwa chini ya uangalizi maalumu wa madaktari kwa muda wa siku
nne ili kuimarisha afya yake.
Akizungumza na Majira alipolazwa
katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) Dar es Salaam, juzi, Lwakatare, alisema
hatua hiyo imefikiwa baada ya madaktari kukutana na kutoa tamko kuhusu matibabu
yake
.
"Nipo chini ya
uangalizi maalumu wa madaktari kwa muda wa siku nne, ambapo ndani ya siku hizo
nne nitakuwa nafanya mazoezi kwa saa tatu kila siku kwa muda tofauti,"
alisema Lwakatare
Lwakatare alisema baada ya
kumalizika kwa hizo siku nne alizopewa; madaktari watamfanyia kipimo cha X-ray
ili kujua kama pingili zitaachana.
Akizungumzia hali yake kwa
sasa, Lwakatare alisema anaendelea vizuri tofauti na ilivyokuwa awali. Alisema
maumivu aliyokuwa akisikia kwenye shingo ni madogo na anaendelea vizuri
Kwa upande wa Ofisa habari
wa MOI, Patrick Mvungi, alisema bado wanaendelea na kumpatia huduma
anayostahili Lwakatare.
Lwakatare alilazwa MOI J uma t a n
o wi k i i l i y o p i t a akisumbuliwa na maumivu makali kwenye shingo ambayo
yalitokana na kusagika kwa pingili za shingo
No comments:
Post a Comment