19 July 2013

KIFAA CHA READYSET KUPUNGUZA GHARAMA YA NISHATI


Na Mwandishi Wetu
WATANZANIAwameshau riw ak utumiaki faachakuchajiainaya Read ySetilikupungu zagharamayanish atipa mojanakujiingizi akipato .Kifaah ichocha kuchaji kilizinduliwan akampun iya mawasiliano y aV odacom,k wakushir ikianana Fen ixInte rna tional Aprilimwak ah uuik iwanalengolakuwa pa tiaWatanzania nishati pa mojanaaji ra .Akizungu mzah ukuaki onyesha kifaa hichojijn iDar esSalaamwi kihii, Me nejawaKampuniyaVo dacom,Nich olus Kizenga, alielezea kuwa Watanzania wamekuwa wakisubiria jambo hili kwa muda mrefu.

“Chaja hizi zimezinduliwa wakati mwafaka kabisa hapa nchini kwa sababu zitaleta msaada mkubwa sana kwa Watanzania walio wengi kwa kuwa zitawasaidia kutunza mali kama pesa na muda,” alisema Kizenga.Kizenga alisema kuwa chaja za ReadySet zimeleta suluhisho la kupunguza gharama ya nishati kwakuwa zinaweza kuchaji simu kumi kwa wakati mmoja, taa za ndani, redio na kompyuta. Alisema kuwa kifaa hicho kinagharimu sh.320,000 na kinaweza kikamuingizia mtu anayefanya biashara ya kuchajisha simu sh.64,000 kwa mwezi.
Alisema kuwa kwa kutumia kifaa hicho pia watumiaji wataweza kujiwekea takribani dola kumi za kimarekani kwa kutokutumia mafuta ya taa.“Watanzania wasiogope kutumia kifaa hicho kwasababu kinaendana na mazingira ya Kitanzania na kinapopata shida kuna mafundi wa kuvitengeneza kwasababu kina uthibitisho,”alisema.
Maneno Mashaka, mmoja wa watu waliokuwepo wakati wa maonyesho hayo, alisema ana matumaini kwamba kwa maendeleo haya, Tanzania inakuwa kiuchumi bila kuwa na gharama kubwa kama za kufungiwa umeme na kuingiza mafuta yatokanayo na petroli nchini.
“Huu ni uzinduzi mkubwa sana, na wengi wetu ambao tulikuwa hatuna umeme majumbani mwetu tumelazimika kutumia mkaa na mafuta ya taa. Haya yametuletea athari kubwa sana za kiafya. Kwa kutumia chaja hizi tunaweza kuingiza kipato na wakati huo huo kupata nishati ya umeme,”alisema Mashaka
Katika uzinduzi huo, ilifahamika kuwa takribani watumiaji milioni 600 wa mitandao ya simu hutumia trilion 16 za Kitanzania kwa mwaka kusafiri kwenda kuchaji simu zao na nishati ya umeme wa betri za magari.

No comments:

Post a Comment