Na Rehema Mohamed
UPANDE wa Jamhuri katika kesi inayomkabili mwanafunzi, Ahsan Ali
Iqbal au Ali Patel (19), raia wa Uingereza na wenzake sita, akiwemo msanii
Chingwele Che Mundugwao, umeomba shauri hilo
liahirishwe hadi kesho ili kuongeza washtakiwa wengine katika kesi hiyo
Mbele ya Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, Wakili wa Serikali Mwandamizi,
Ladslaus Komanya, alidai shauri hilo
lilifikishwa kwa ajili ya kutajwa, hivyo aliomba liahirishwe kwa muda fupi hadi
kesho ili kuunganisha washtakiwa hao na wengine.
Mbali ya Patel na Che Mundugwao, washtakiwa wengine ni ofisa ugavi
wa Idara ya Uhamiaji, Shemweta Kiluwasha, Injinia Kenneth Pius wa Kikosi cha
Zimamoto na Uokoaji, mfanyabiashara Ally Jabir, Rajabu Momba na Haji Mshamu.
Wa s h t a k iwa h a o amb a o wanakabiliwa na mashtaka ya kula
njama, wizi wa hati 26 za kusafiria mali
ya serikali, kughushi, kuwasilisha hati ya kughushi walipanda kizimbani jana
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu shauri hilo lilipotajwa.
Komanya alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado unaendelea na
kwamba wanaomba liahirishwe hadi kesho.
Hakimu Sundi alikubali ombi hilo
na hivyo aliahirisha kesi hiyo na washtakiwa hao kurudishwa rumande hadi kesho.
No comments:
Post a Comment