17 July 2013

KESI YA GHOROFA LILILOANGUKA DAR YAAIRISHWA


 Na Rachel Balama
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imeahirisha kesi ya mauaji bila ya kukusudia inayowakabili washtakiwa 11 yaliyohusisha jengo la ghorofa 16 lililoanguka hivi karibuni katika Mtaa wa Indragandi na kuhusisha vifo vya watu zaidi ya 30 kutokana na kutokamilika kwa upelelezi.
Kesi hiyo inamkabili mmiliki wa jengo hilo Bw. Raza Ladha na wenzake 10 ambao wanakabiliwa na mashtaka 24 ya mauaji bila kukusudia.

Hakimu Devota Kisoka liiahirisha kesi hiyo hadi Agosti 15, mwaka huu itakapotajwa tena baada ya Wakili wa serikali Genes Tesha kuieleza mahakama kwamba upelelezi haujakamilika.
Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Bw. Goodluck Mbanga, Bw. Wilbroad Mugyabaso, Bw. Ibrahimu Mohammed, Bw. Mohamed Abdulkarim ambaye ni injinia na Bw. Charles Ogore pia ni injinia.
Wengine ni mhandisi mshauri Bw. Zonazea Mashudada, msanifu majengo Bw.Vedasto Fednand, Bw. Michael Hema, ofisa mtekelezaji Bw.Joseph Ringo na msajili msaidizi Bw. Halbert Munuo.
Ilidaiwa kuwa washtakiwa hao walitenda kosa hilo Machi 29, mwaka huu maeneo ya Mtaa wa Indragandi wilayani Ilala jijini Dar es Salaam.
Washtakiwa hao wanadaiwa kuua bila kukusudia ambapo watu wanaodaiwa kuwaua kuwa ni Yusufu Sharifu, Kulwa Khalfani, Hamad Musa, Kessy Ally, Hamisi Mkomwa, Boniface Benard, Suhail Karim, Salma Akbar, Selemani Haji, Selemani Mtego na Sikudhani Mohammen.
Wengine ni Ahmed Mirambo, Salum Mapunda, Selemani Mnyoni, John Majewa, Mussa Munyamani, David Helman, Willium Joackim, Abdulrahman Othman, Emanuel Christion, Mmanyi Ngadula, Advai Desiki, Emanuel Watiani na Augustino chuma.  

No comments:

Post a Comment