16 July 2013

JWTZ WANNE HALI MBAYA DARFUR


 Na Rehema Mohamed
HALI ya askari wanne wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kati ya 14 waliojeruhiwa katika shambulio la waasi mjini Darfur nchini Sudan ni mbaya na wapo chini ya uangalizi wa madaktari.
Akizungumza na gazeti hili jana Msemaji wa JWTZ, Kanali 
Kapambala Mgawe, alisema majeruhi 10 hali zao zinaendelea vizuri na kwamba wanaweza kujihudumia wenyewe mambo madogo madogo, kwamba wanaweza kutembea na kuzungumza
.

A l i s ema ma j e r u h i h a o wanaendelea na matibabu eneo la Nyara kwenye Hospitali Kuu iliyopo eneo la operesheni.
Akizungumzia hatua iliyofikiwa kurudisha miili ya wanajeshi saba waliouawa katika shambulio hilo, alisema taratibu hizo zipo chini ya Umoja wa Mataifa (UN) hivyo bado wanalifuatilia.
“Suala la kuwarudisha askari saba waliouawa lipo chini ya UN na tunafuatilia,”alisema Kanali Mgawe. Mapema wiki hii JWTZ ilitoa taarifa kuhusu askari wake hao kuuawa na wengine kujeruhiwa katika shambulio la kushtukiza ambalo lilifanywa na waasi wa Sudan Julai 13, mwaka huu.
A s k a r i h a o w a l i k u w a wakiwasindikiza waangalizi wa amani kutoka Khor Abeche kwenda mjini Darfur.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, shambulio hilo lilitokea umbali wa kilomita 20 kutoka Makao Makuu ya kikosi hicho ambapo miongoni mwa waliojeruhiwa ni pamoja na maofisa na askari kutoka mataifa mengine.
Wakati kikosi cha askari jeshi wa Tanzania kikishambuliwa, kilikuwa na askari 36 ambao ni miongoni mwa askari wanaolinda amani kwenye Kikosi cha UN mjini Darfur nchini Sudan.

No comments:

Post a Comment