19 July 2013

JWTZ WALIOUWAWA DARFUR KULETWA KESHO



Na Mwandishi Wetu

MIILI ya askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha katika Jimbo la Darfur nchini Sudan kutokana na shambulizi la ghafla, itawasili kesho kwa ndege maalum katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Terminal one jijini Dar es Salaam. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi, Upanga jana ilieleza kuwa shughuli ya kupokea miili ya wanajeshi hao itaanza saa nne asubuhi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa mara baada ya kuwasili miili hiyo itapelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Jeshi, Lugalo, baada ya maandalizi ya miili hiyo, tarehe na utaratibu wa kuaga kwa heshima zote zitafuata.Askari hao waliuawa wakiwa wanawasindikiza waangalizi wa amani kutoka Khor Abeche kwenda mjini Darfur. Katika shambulio hilo askari wengine wa Tanzania 14 walijeruhiwa. Shambulio hilo lilitokea umbali wa kilometa 20 kutoka Makao Makuu ya kikosi hicho ambapo miongoni mwa waliojeruhiwa ni pamoja na maofisa na askari kutoka mataifa mengine.

Wakati kikosi cha askari jeshi wa Tanzania kikishambuliwa, kilikuwa na askari 36 ambao ni miongoni mwa askari wanaolinda amani kwenye Kikosi cha UN mjini Darfur nchini Sudan.

No comments:

Post a Comment