Na Juma Kiyenze
TANZANIA
imeadhimisha miaka 50 ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) mwaka huu, tangu
lilipoanzishwa kisheria Julai 10 mwaka 1963 chini ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu
wa Kwanza, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na washirika wake.
Lengo la kuanzishwa kwake kulilenga kujenga umoja
wa kitaifa, kuwapatia mafunzo ya kijeshi na stadi za kazi vijana
ukakamavu na uzalendo katika nyanja
mbalimbali za uchumi, jamii, kilimo, ulinzi na usalama wa taifa.
Malengo mengine
ilikuwa ni kujenga mshikamano, udugu, kujitegemea, kuongeza ufanisi wa kazi,
nidhamu, kujituma na kuwaandaa kulitumikia taifa kupitia vyombo vza ulinzi na
usalama, sanjari na sekta binafsi kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.
JKT ilifanikiwa
kutimiza malengo yake kitaifa na kimataifa kuwakomboa wananchi kiitikadi,
kielimu, kisaikolojia, kiutamaduni, kiutendaji na kwamba hakukuwa na ubaguzi
ulioruhusiwa kuota mizizi miongoni mwa jamii.
Kufanikiwa
kwake kulitokana na uadilifu wa viongozi waliopewa dhamana kuongoza JKT kwa
nyakati mbalimbali, ambao walishirikiana na watendaji wake kutimiza wajibu wao
kulingana na dhamana walizokabidhiwa kwa uaminifu, uadilifu, ubunifu,
uvumilivu, kujituma, ujasiri na nidhamu.
Wananchi
walijenga imani kubwa kwa jeshi lao kulingana na jinsi lilivyokuwa limejipanga
katika nyanja mbalimbali kutekeleza majukumu ya Serikali katika suala zima la
malezi ya vijana na uzalishaji mali.
Historia ya JKT
Watanzania
watakumbuka kwamba, miongoni mwa taasisi zilizoanzishwa na Serikali ya
Tanganyika, baada ya uhuru Desemba 9, 1961 ni JKT, ili kuepusha athari
zilizoachwa na Wakoloni zisilete madhara miongoni mwa jamii.
Athari hizo ni
ubaguzi, udini, ukabila, rangi na tofauti ya kipato, hatua ambayo ilifanikiwa
kutokana na taifa kuwaelimisha na kuwaandaa vijana kupitia vikosi na makambi
mbalimbali za malezi na mafunzo chini ya jeshi hilo.
Taasisi hiyo ina wajibu kuhakikisha
maendeleo ya nchi yanafikiwa katika sekta ya uzalishaji mali kupitia sekta ya
kilimo, ili kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa kutoa mafunzo zaidi ya
ujasiriamali vikosini.
Kuanzishwa kwake kulitokana na mawazo ya
Hayati Mwalimu Nyerere na Mzee Rashid Mfaume Kawawa (Simba wa Vita), ambao kwa
pamoja waliona ipo haja ya kuanzisha taasisi itakayokuwa na jukumu la kuwapatia
vijana malezi na kuwaandaa kiutendaji makambini.
Walipoafikiana mawazo yao yalipelekwa kwa
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Tanganyika African National Union
(TANU Youth League), Hayati Joseph Nyerere, ambaye naye aliyafikisha katika
Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika mkoani Tabora Agosti 25, mwaka 1962.
Mkutano huo uliafiki mawazo ya viongozi
hao na Aprili 19 mwaka 1963, Baraza la Mawaziri la Tanganyika chini ya Rais wa
Jamhuri ya Tanganyika, Mwalimu Nyerere, lilipitisha azimio la umoja huo.
Mnamo Julai 10 mwaka 1963 JKT ilianza
kutekeleza majukumu yake kwa kuwachukua vijana kutoka mikoa mbalimbali ya nchi
kujiunga na jeshi hilo na kundi la awali la vijana 11 kutoka wilaya 11 walipata
mafunzo Kambi ya JKT Mgulani Dar es Salaam.
Vi j a n a h a o wa l i k uwa n i Makatibu
wa Umoja wa Vijana wa TANU, ambao walipelekwa nchini Yugoslavia mwaka 1962 kwa
mafunzo ya uongozi wa vijana, Bi. Z. Kiango, Bw. S. Chale, Bw. P. Lwegarulira,
Bw. R. Kamba, Bw. H. Ngalason na Bw. J. Ndimugango (wote sasa hawapo jeshini).
Wengine ni pamoja na Bi. M. Mhando (Senior
Guide), Bw. DS. Msilu (Master), Bw. ES. Mwakyambiki (Senior Master), AI. Msonge
(Master) na Bw. LM Mitande (hawa wangali katika Jeshi la Kujenga Taifa.)
Mnamo Agosti 1963 kikundi kingine cha watu
watano kilijiunga JKT na kupatiwa mafunzo ya uongozi wa vijana jeshini ni Bw.
S. Desai, Bw. E. Simkone, Bw. J. Mwanimlele (Asst Master) na Bw. A A Moyo (Asst
Master).
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa JKT, Mwalimu
Nyerere aliwaambia wananchi kuwa, umuhimu wa jeshi hilo unatokana na Taifa
kuhitaji huduma ya vijana kulitumikia Taifa lao katika majukumu mbalimbali
yatakayotolewa ama kujitokeza kijamii, kiuchumi, kielimu na kiitikadi.
Pamoja na hayo, mwaka 1964, ilitungwa
Sheria ya JKT (National Service Act), ambayo ilianzisha mafunzo kwa Mujibu wa
Sheria na mwaka 1966 na 1967 sheria ilifanyiwa marekebisho kuwawezesha vijana
waliokuwa wanahitimu elimu ya upili kidato cha nne na sita kujiunga katika
mafunzo yake.
Kufuatia marekebisho hayo, yalitoa fursa
kwa kundi la kwanza la vijana 11 kujiunga na JKT kwa Mujibu wa Sheria
Operesheni Azimio la Arusha
Kundi la viongozi mbalimbali wa kitaifa
lilijiunga mwaka 1968 kwa mafunzo maalum ya uongozi wa JKT, ambao walikuwamo
Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Makamu wa Kwanza wa Rais,
Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, Makamu wa Pili wa Rais na Waziri Mkuu Hayati Rashid
Mfaume Kawawa na Spika wa Bunge la Jamhuri Hayati Chifu Adamu Sapi Mkwawa,
ambalo lilikuwa Operesheni Kazi “A“.
Mwaka 1975, JKT iliunganishwa na Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ingawa majukumu ya msingi yalibaki ndani
ya jeshi hilo, ikiwa ni Brigedi ya uzalishaji ya Jeshi.
Athari za
mtikisiko wa uchumi duniani
Kutokana na kuyumba kwa uchumi duniani wa
nchi zilizoendelea kwa viwanda barani Ulaya na Marekani katika miaka ya 1980 –
1995, nchi nyingi changa zilizokuwa zinaendelea, ikiwamo Tanzania ziliathirika
kiuchumi.
Serikali ililazimika kusitisha shughuli za
JKT mwaka 1994 hadi 2001 kwa vijana kwa mujibu wa sheria na kupunguza shughuli
zake.
Kusitishwa kwa mafunzo ya JKT, athari
nyingi zilijitokeza miongoni mwa jamii, ikiwa ni pamoja na mmomonyoko wa
maadili kwa viongozi, watendaji mbalimbali, nidhamu, kuongezeka kwa vitendo
viovu mitaani, wizi, uvutaji bangi, ubwiaji wa dawa za kulevya, ubakaji,
ujambazi na ubaguzi uliongozeka na kuleta fedheha kwa nchi.
Kulingana na kuwepo kwa hali hiyo,
viongozi wa JKT walikabiliana na mazingira hayo na changamoto mbalimbali
zilizojitokeza, sanjari na kufutwa kwa jeshi hilo.
Hali hiyo ilitokana na ushawishi wa
mataifa yaliyokuwa yanatoa misaada katika nyanja mbalimbali za jamii kwa
viongozi wa kitaifa waliokuwa na dhamana ya madaraka, ambayo walitaka JKT
ifutwe ama ishushwe hadhi.
Serikali ilikataa mawazo hayo yaliyolenga
kuparaganisha taifa, ili kutoa mwanya wa kujipenyeza kuotesha upya mimea ya
ubaguzi, udini, ukabila na vitendo vingine kwa jamii.
Tume maalumu ya wataalam iliyoteuliwa na
Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Makame Rashid wakati huo ilifanya kazi yake vyema na
kuishauri serikali kutofanya ajizi kufuta jeshi hilo, kwani athari zake
zingekuwa kubwa na hatari zaidi.
Kufungwa kwa makambi
Mtikisiko wa uchumi duniani uliathiri
shughuli mbalimbali, hivyo ulichangia kambi za JKT za kilimo na ufugaji
kufungwa, ikiwa ni pamoja na Luwa mkoani Rukwa, Msange- Tabora, Mpwapwa-Dodoma
na Makuyuni-Arusha.
Kambi hizo zilitumika kutoa mafunzo ya
kilimo na ufugaji kwa nadharia na vitendo vijana waliokuwa wanajiunga na JKT
kila mwaka kwa mkataba maalum, hivyo ziliathiri majukumu yake na miundombinu
yake iliharibika.
Kuzinduliwa kwa
mafunzo
ya JKT
Machi 26 mwaka huu mafunzo ya JKT kwa
Mujibu wa Sheria, yalizinduliwa upya, baada ya kusimamishwa kwa zaidi ya miaka
19 na Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete.
Mafunzo hayo ambayo yalikuwa ya wiki tatu
kwa Kundi Maalum la wabunge 22 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
miaka miwili ya kujitolea Operesheni Miaka 50 ya JKT Kambi ya JKT Ruvu mkoani
Pwani.
Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi wa
kitaifa waliowahi kupitia mafunzo ya jeshi hilo katika kambi hiyo kwa Mujibu wa
Sheria Operesheni Tumaini mwaka 1972, ambaye alikuwa Kombania ‚A‘ akipatiwa
namba ya JKT 9983.
Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Raphael Muhuga
alimwambia Amiri Jeshi Mkuu kwamba, mafunzo ya miezi mitatu yalianza Machi 4,
mwaka huu Kambi za JKT Bulombora- Kigoma, Msange-Tabora, Ruvu- Pwani na
Mgamboa-Tanga, ambayo yaliwashirikisha vijana 5,000 kati ya 41,000 waliohitimu
elimu ya upili kidato cha sita mwaka huu na yaligharimu Shs 7.5 bilioni.
Akizungumzia wabunge anasema walioomba
kujiunga JKT ni 47, jumla ya 24 walikwenda katika kambi walizopangiwa na 22
walihitimu, wawili hawakufaulu kutokana na sababu mbalimbali za kiafya.
Dira ya JKT
Dira ya JKT inataka Tanzania iwe nchi ya
watu waliolelewa vyema kitaifa na kujengwa katika misingi ya nidhamu,
kujiamini, moyo wa uzalendo, umoja na udugu, kupenda kazi na kutekeleza wajibu,
tayari kuitumikia nchi yao katika suala zima la uchumi, elimu, ulinzi na usama.
JKT inaendeshwa kwa kufuata misingi,
maadili ya kujenga umoja na mshikamano wa kitaifa, ambayo ni uadilifu,
kujitolea, mshikamano, umoja, uzalendo, nidhamu na kufanyakazi.
Mafanikio yake kwa taifa
JKT ilifanikiwa kuimarisha umoja wa
kitaifa, ambapo vijana mbalimbali waliohitimu mafunzo hayo walijituma
kufanyakazi za mikono kwa kujiheshimu, walikuwa viongozi mahiri, wavumilivu,
wabunifu na walithamini kuhifadhi utamaduni wa taifa.
Jeshi hilo limechangia kuimarisha michezo
mbalimbali na kuiletea sifa Tanzania kitaifa na kimataifa, pia vijana walikuwa
mstari wa mbele kuokoa jamii katika majanga ya asili yaliyotokea kwa vipindi
tofauti hapa nchini.
Taasisi hiyo ni mfano wa kuigwa kutokana
na mataifa mbalimbali duniani kufika nchini kujifunza shughuli zake na wao
kuanzisha JKT katika nchi zao, ikiwamo JKU Zanzibar, Zambia na Guyana.
Hifadhi ya mazingira imepewa kipaumbele
kwa kutambua umuhimu wake kwa maisha ya jamii na wanyama, hivyo JKT hugawa
miche bure kwa wananchi waishio jirani na kambi, sanjari na kubadilishana
uzoefu na utaalamu wa suala zima la utunzaji na uhifadhi wake.
Naishauri Serikali itoe fedha zinazokidhi
mahitaji ya JKT na kutembelea mara kwa mara kuona utekelezaji wa majukumu yake
vikosini, pia kuwabaini watendaji wasiowaadilifu kiutendaji, ambao hufanya kazi
kwa masilahi yao na sio kwa jeshi hilo na taifa kwa ujumla.
Watendaji wengi wanaichukulia JKT kuwa ni
sehemu ya kujilimbikizia mali na kusahau majukumu yake, hivyo kusababisha jeshi
hilo kuonekana halifai, kumbe baadhi ya viongozi wanaoteuliwa ni butu
kiutendaji.
Kuundwa kwa JKT Staff SACCOS ni sehemu
muhimu ya mafanikio ya JKT, ambayo ililenga kuwawezesha watendaji wake
kuimarika kiuchumi na kuepuka kukopa katika taasisi za fedha ambazo hutoza riba
kuba.
Mwitikio ulikuwa ni mzuri kwa maofisa,
askari na watumishi wa umma, ingawa ushirika huo haujakomaa kutokana na uchanga
na ubovu wa baadhi ya watendaji na wanachama kutokuwa waaminifu kiutendaji,
hivyo kusimama na kuwa sehemu ya changamoto zilizopo JKT, tangu kuundwa kwake
miaka 50 iliyopita.
Naamini viongozi hili wameliona na
litafanyiwa kazi, ili ushirika huo uweze kuendelea kuwahudumia wanachama wake,
kuwakomboa katika dimbwi la umaskini uliokithiri na wengine kujiunga zaidi, ili
kuleta ushindani wa kibiashara na kuaminiwa na jamii.
JKT Staff Saccosni kimbilio la wanyonge
walio wengi, uboreshaji na utendaji wake unahitaji watu walio makini
kiutendaji, ili iweze kutekeleza agizo la Serikali kuwapatia wanachama mikopo
ya kilimo kufanikisha mapinduzi ya kijani.
Operesheni za Vijana JKT
JKT mpaka sasa imekwishaendesha zaidi ya
operesheni 102, kwa takwimu ya wakati huo ni Ujenzi 1980, Tija 1980, Juhudi
1981, Imarisha 1981, Tekeleza “B” 1982, Kujihami 1982, Safisha1983, Nguvu Kazi
1983 na Mshikano 1984.
Zingine zilikuwa ni wajibu 1984, Vijana
1985, Okoa 1985, Awamu ya Pili 1986, Nidhamu 1986, CCM Miaka 10 1987, Miaka 20
ya Azimio la Arusha 1987, Kizota 1988, Miaka 25 ya JKT 25 YA JKT 1988, Mpito
1989, Program ya Chama 1989 na Kambarage 1990/91.
Julai 10 mwaka huu ni kilele cha
maadhimisho ya JKT kutimiza miaka 50 tangu liundwe mwaka 1963 na shamrashamra
mbalimbali zimefanyika katika makambi na vikosi hapa nchini.
JKT kutimiza umri wa nusu karne sio kazi
rahisi, hivyo muda umefika kwa viongozi wasiowajibika kujivua magamba kabla ya
kusubiri kuvuliwa, ili kupisha wachapa kazi watakaowezesha jeshi hilo kusimama
imara miaka 50 ijayo.
Muda huu utumike kuona changamoto
zilizopita, zilizopo na zijazo na jinsi ya kupambana nazo kijeshi, ambayo
huchangia kustawisha tija na ufanisi endelevu JKT na maamuzi ya siasa yaepukwe,
kwani hudumaza maendeleo.
Hata hivyo Taifa la Israel lilisaidia
uanzishwaji wa JKT miaka 50 hapa nchini ambapo ilitoa wataalamu mbalimbali na
walipokamilisha majukumu yao walirejea nchini mwao.
JKT ilifuata mfumo wa uongozi wa Israel na Tanzania
ilipeleka watu nchini humo kujifunza taaluma mbalimbali za malezi ya
vijana,uendeshaji uongozi na
No comments:
Post a Comment