Na
Mwandishi Wetu
SERIKALI imewatoa hofu Watanzania
ikiwataka kutosita kujiunga na kutumia huduma za kifedha zinazofuata kanuni za
Kiislamu ikiitaja huduma hiyo kama mkombozi kwa wananchi walio wengi.Akizungumza
wakati wa hafla ya futari kwa wateja iliyoandaliwa na Benki ya Taifa ya
Biashara (NBC) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Naibu Waziri wa Fedha,
Bi. Saada Mkuya Salum alisema bidhaa hiyo imeletwa katika muda mwafaka.
"Huduma
hii hufuata sheria na kanuni za Kiislamu. Ni huduma inayojali na kufuata
maadili na ni furaha kwa Serikali kuona kwamba hatimaye maadili sasa yanaingia
hadi kwenye huduma za kifedha."Maadili
yakiwa imara katika jamii, tunatarajia pia kupata uchumi imara wenye kukua na
viwanda vyenye kuzalisha bidhaa na huduma zenye kukidhi mahitaji ya wote,"
alisema.
Bi.
Saada aliiomba NBC kuendelea kubuni na kuwaletea Watanzania huduma nyingine
zenye kukidhi mahitaji mbalimbali ya wateja, wakubwa kwa wadogo, hususan mikopo
kupitia huduma ya kibenki ya Kiislamu.Aliitaka
pia benki hiyo kutoa elimu kwa Watanzania ili waweze kufahamu kiundani faida ya
huduma hiyo ambayo iko wazi kwa yeyote bila kujali itikadi au imani yake ya
kidini.
"Ni matumaini
yetu kwamba wengi watafaidika kutokana na huduma hii, hasa mtakapoanzisha
huduma ya mikopo isiyo na riba kwa mujibu wa kanuni za Kiislamu," alisema.Akizungumza wakati wa
hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Bi. Mizinga Melu alimuahidi Naibu
Waziri kwamba benki hiyo haitaacha mipango yake ya kuisaidia Serikali
kutekeleza kauli mbiu yake ya 'maisha bora kwa kila Mtanzania'. "Tumejizatiti
katika hili na kama unavyojua na sisi kauli mbiu yetu ni maisha bora kwa kila
mtanzania hivyo tutayatumia matawi yetu yaliyoenea nchi nzima kuwafikia
Watanzania kokote waliko na kuwapelekea huduma bora za kifedha ambazo
hawajawahi kuzipata wakati wowote," alisema.
Naye Mkuu wa Kitengo
cha Huduma ya Kibenki ya Kiislamu, Bw. Yassir Masoud lisema kuwa muda si mrefu
NBC itaanzisha huduma za mikopo kupitia bidhaa hiyo, akisisitiza kwamba wanaelewa
kuwa watu wengi wanaisubiri kwa hamu kubwa.
Aidha Huduma ya Islamic Banking ya Benki ya NBC ilizinduliwa mwezi Mei
mwaka 2010 hapa nchini.
Je huu si udini? Je ifunguliwe Christian Banking? Hii ni nchi isiyo na dini . Raisi Kikwete Unaipeleka wapi Tanzania hii. Ukiwa mwislamu unayeingiza mambo ya Udini. hatupUarabu. Tuko Tanzania hapa au umesahau kama inatakiwa uwe Raisi wa bila dini yeyote? Pia kwenye Vyama. Ulikemea Chadema na mafunzo kwa Vijana wao. Mbona umekaa kimya kwa CCM? jambo jingine Kama Amiri Jeshi, matukio yote ya mauaji hadharani kupitia vyombo vya dola, Umeshindwa kutoa tamko kwa Polisi, JwT, na bomu ambalo jeshi lako la polisi wakisingizia limetupwa kwa makosa. Sasa wewe ni kiongozi wa Amani au vipi? Kama umezidiwa na jeshi au unaliogopa kwa nini usijiuzuru ukaiacha nchi kwa amani. Wapishe wenye moyo wa kuipigania nchi hii na kuleta maendeleo na amani kwa wote. Jeshi unalo na sasa majambazi yanateka mabasi. Lakini upo busy mitaani kwa mambo yasiyo na uzito kila siku. Naona umezidiwa na kazi, basi omba msaada ukapumzike. Taifa linaangamia na huku uko mitaani kukunena yasiyo na msingi. Umetawala mda mrefu, na umefanya mabadiliko mengi na unashindwa kuyamudu.
ReplyDelete