Na
Mwandishi wa EANA
KATIBU Mkuu wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dkt. Richard Sezibera, ameelezea umuhimu wa
kuifanya jumuiya hiyo kuwa yenye msisimko zaidi na ya kuvutia." J umu i y a y
e t u ( EAC) inatakiwa kuwa ya manufaa, yenye ufanisi, msisimko na ya kuvutia
kuwawezesha wana Afrika Mashariki kupata kilicho bora kutoka kwake." Dkt. Sezibera alitoa
kauli hiyo wakati akizindua utafiti juu ya uelewa wa raia wa Afrika Mashariki
kuhusu mtangamano wa Jumuiya hiyo, unaofanywa kwa ushirikiano baina ya EAC na
Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Ujerumani (GIZ) katika nchi tano wanachama
wa jumuiya hiyo.
Hafla hiyo
ilihudhuriwa na timu ya watafiti na maofisa waandamizi wa GIZ. Utafiti huo
utakaofanywa katika nchi wanachama ambazo ni Burundi,Kenya,Rwanda, Tanzania na
Uganda utachukua mwezi mmoja na unatarajiwa kumalizika Agosti 24.
Utafiti huo
utafanyika kwa njia ya madodoso ya kwenye mtandao na kwa mahojiano ya moja kwa
moja katika maeneo maalum yatakayochaguliwa kwenye majiji na miji ya mipakani."Utafiti huo
unatarajiwa kutupatia mwanga juu ya namna ya watu wanavyoiona EAC,
wanavyoifahamu vizuri, jinsi wanavyozifahamu nembo za EAC na jinsi
wanavyotathmini utendaji wake," alisema.
Kwa mujibu wa taarifa
ya EAC, kubwa zaidi katika utafiti huo ni kutathmini jinsi taarifa
zinavyowafikia walengwa na jinsi inavyoeleweka na raia wa Afrika Mashariki na
namna gani ya kuweza kusonga mbele.
Dkt. Sezibera
alipongeza juhudi za utafiti, akisema zipo katika uhalisia wa kutaka kuileta
jumuiya hiyo karibu zaidi na walengwa.Mkuu wa Mawasiliano na Masuala ya Umma wa EAC, Owora Othieno, alisema
mradi huo unalenga kubaini kama ndoto za
mtangamano za wana Afrika Mashariki zinaendana na matakwa ya Mkataba wa EAC.
No comments:
Post a Comment