Na Heri
Shaaban
WAMILIKI wa Daladala Mk o a wa Da r e s
Salaam (DARCOBOA) wameanzisha Kampuni mbili zitakazoagiza magari kwa ajili ya
Mradi wa Mabasi Mwendo Kasi (DART) kwa ajili ya kutoa huduma jijini Dar es
Salaam.Wamiliki
hao wa DARCOBOA walifikia hatua hiyo ya kuunda kampuni zao Dar es Salaam jana,
baada ya Serikali kuwapa waraka wa kusimamia mradi huo kwa sharti la kuwa
wameanzisha kampuni inayotambulika. Akizungumza
katika kikao cha wamiliki wa daladala jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa
DARCOBOA, Sabri Mabouk, alisema lengo la kuunda kampuni hizo mbili ni
kuwawezesha kutambulika ili kuweza kuagiza magari kutoka nje ya nchi yasiozidi
300.
"Kampuni
zetu mbili moja itakuwa ofisi zake Ubungo katika kituo cha mabasi ya mikoani
kwa sasa nyingine Jangwani. Alisema kila mmiliki wa daladala anatakiwa kujiunga
katika kampuni hii ili aweze kuchangia hisa zitakazofanikisha mradi huo.Sabri
alisema hatua ya kuanzisha kampuni hiyo ni dhamana waliyopewa na Rais Jakaya
Kikwete, akitaka huduma hiyo isimamiwe na wamiliki wa DARCOBOA na sio uvumi wa
maneno ya mitaani kuwa kampuni za wafanyabiashara wakubwa wamechukua tenda
hiyo.
Alisema ifikapo
Desemba mwaka huu kampuni hizo zitakuwa zimetambulika pamoja na usajili wake
ili waweze kuagiza magari kutoka nje kazi itakayochuka mwaka mmoja ili magari
yaweze kufika nchini."Wamiliki wa
daladala Dar es Salaam tupo 5,000 hadi 6,000 kama DARCOBOA tumeweka kiwango cha
kuchangia hisa ya sh. milioni 1.5 kila mmiliki ili tuweze kupata sh. bilioni 5
zitakazokuwa mtaji wa kuagiza mabasi hayo jambo ambalo
linawezekana,"alisema.
Alisema katika
barabara ya Morogoro mabasi 300 yatatoa huduma hiyo na mabasi 150 ofisi zake
zitakuwa Jangwani na mengine 150 ofisi zake zitakuwa Ubungo.Aliwataka wamiliki wa
daladala ambao bado hawajajiunga kwenye umoja huo kufanya haraka ili waweze
kupata fursa hiyo. Alisema watakaoshindwa kujiunga katika kampuni hiyo
watashindwa kusafirisha abiria katika Barabara ya Morogoro, kwani mradi huo
ukianza katika njia hiyo unatarajia kuondoa wastani wa daladala 1,200 hadi
1,500 hivyo kulazimika kusubiri awamu ya pili katika Barabara ya Kilwa. Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa DARCOBOA, Mashaka Karume, aliwataka
wamiliki wa daladala kuwa kitu kimoja na kujenga tabia ya kuaminiana ili waweze
kupata kiasi hicho cha fedha wanachokusudia
No comments:
Post a Comment