Na Allan Ntana, Tabora
UONGOZI wa Benki ya CRDB tawi la Tabora umesema utaendelea
kuheshimu na kuthamini misingi ya maadili na imani za wateja wake kwa kuunga
mkono utekelezaji wake. Meneja wa tawi la CRDB Tabora, Sdney Bakari alisema hayo kwenye
taarifa yake aliyoisoma kwenye hafla ya futari ilifanyika katika Ukumbi wa Chuo
cha Utumishi wa Umma,(TPSC) tawi la Tabora.
Bakari alisema hafla hiyo ya futari ya mwezi Mtukufu wa Ramadhan
kwa waumini wa dini zote ni miongoni mwa ushiriki wa Benki ya CRDB kwani benki
hiyo imeshafanya shughuli nyingi za kijamii kwa kushirikisha taasisi kadhaa. Aidha, meneja huyo alisema CRDB imeshafanya shughuli hizo ikiwa ni
pamoja na misaada ya vifaa na vyakula kwa taasisi zinazosaidia makundi ya watu
wenye uhitaji.
"Makundi ambayo hadi sasa CRDB imekuwa ikitoa misaada na
kushiriki kwenye shughuli mbalimbali ni yatima,wagonjwa,waliokumbwa na majanga
na walemavu," alisema Bakar. Alisema benki hutenga kiasi kidogo cha faida yake kusaidia jamii
na hii imekuwa ni moja ya sera za benki kila mwaka kwani wanathamini mafanikio yao yanayotokana na
wateja wake na jamii inayowazunguka.
Akizungumzia baadhi ya huduma zake kwa wateja wake alisema,
wameamua kusogeza huduma ijulikanayo kama 'Fahari Huduma' ambayo ni huduma
inayomwezesha mteja wa CRDB kupata huduma za benki kama
kujua salio, kuweka na kutoa fedha, kupokea fedha, kutuma fedha na huduma za
ufunguaji akaunti kupitia mawakala maalumu. Bakar alisema zaidi ya hapo hadi sasa CRDB imeendelea kutanua wigo
ili kusogeza huduma kwa wateja wake ambapo hadi sasa wanatarajia kufungua
matawi wilaya za Sikonge na Urambo huku kukiwa na tawi jipya lililoanzishwa
hivi karibu mkoani hapa.
Katika hafla hiyo meneja huyo alisema kuwa wanatarajia kuchangia
kiasi cha sh milioni 2 kuchangia shughuli za Baraza Kuu la Idd linalotarajiwa
kufanyika kitaifa mkoani Tabora. Naye Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Shaban Salum katika salamu
zake aliipongeza Benki ya CRDB kwa hatua hiyo muhimu ya kuungwa mkono najamii
nzima.
Shekhe Salum alisema sehemu ya hiyo ya hafla ya futari iwe ni
sehemu ya kumtaka Mwenyezi Mungu msamaha ili tupate malipo, heri nyingi na
Baraka. Alisema mwenyezi Mungu alituletea
mwezi bora na tuwe waungwana naye atusamehe zambi zetu.
No comments:
Post a Comment