Na Jamillah Daffo, babati
MWENYEKITI wa Umoja
wa Wanawake Taifa (UWT) wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sophia Simba, amewataka
wanachama wa chama hicho wasivunjike moyo kwa kupoteza viti vya udiwani katika
uchaguzi mdogo uliofanyika hivi karibuni.Simba
ambaye pia Waziri wa Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto, aliyasema hayo juzi
katika ziara yake wilayani Babati ambapo ameambatana na Katibu Mkuu wa UWT
Taifa, Amina Makilag
Katika
uchaguzi huo, ambapo aliongea na viongozi wa ngazi ya mkoa na wilaya katika
ofisi ya Katibu wa CCM Mkoa wa Manyara na baadaye aliongea na wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Old-Majengo mjini Babati.Katika
uchaguzi huo CCM ilishindwa katika kata mbili za Bashnet iliyopo Babati
Vijijini na Dongobeshi Wilaya Mbulu, ambapo CHADEMA iliibuka mshindi.
"Poleni
kwa kushindwa kwani ilituuma sana, kwa kushindwa
kule tunapigiwa kengele tusicheze kabisa ingawa sote tunajua chaguzi ndogo watu
hawaendi kupiga kura sisi hilo
linaweza likatuathiri pia na hali iliyotokea mkoani Arusha," alisema na
kuongeza;"Ndugu
zangu tusifanye mambo yetu gizani tutakuwa hatukitetei chama chetu, tutakwenda
na maji."
Alisema
pamoja na kujitahidi kufanya kampeni nyingi lakini walishindwa katika uchaguzi
huo mdogo na badala yake kata kuangukia CHADEMA.Alisema
hiyo ni dalili mbaya, hivyo wana-CCM wanatakiwa kujipanga upya ili kuondoa hali
hiyo.
"Lazima
tuwe na watu wetu ndani mwao ikiwezekana tuwalipe kwani wao wana watu wao ndio
maana wanajua mbinu zetu,"alisemaAliwataka
viongozi kuhakikisha wanakuwa karibu na wanachama ili ule unyonge
uliosababishwa na vuguvugu la chaguzi ndogo uondoke, kwani wana-CCM hawajui
kujibu mapigo bali hujipanga kuhakikisha pale walipokosea wanajirekebisha.
Kwa
upande wake Katibu Mkuu wa UWT Taifa, Makilagi, alisema mara nyingi wanawake
wamekuwa wakishindwa kujiamani na uwoga unachangia kushindwa kutekeleza wajibu
wao katika nafasi zao za uongozi.Naye
Katibu wa UWT Mkoa wa Manyara, Salome Luhinguranya, alisema ziara ya waziri
inawezekana ikaleta mabadiliko na chachu katika mkoa huo ambao unaendelea
kutekwa na wimbi la upinzani.
Alisema ni wazi wapinzani wame j i a n d a a k u
h a k i k i s h a wanashinda kwa nguvu
No comments:
Post a Comment