12 July 2013

BONDIA CHEKA KUPIGA KAMBI KENYA


 Na Halfan Diyu, Morogoro
BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Francis Cheka 'SMG' anatarajia kuweka kambi ya wiki nne nchini Kenya kwa ajili ya kujiandaa na pambano lake la ubingwa wa Dunia, uzito wa kati.
Pambano hilo linalosimamiwa na Shirikisho la Kimataifa la Ngumi (WBF) litafanyika Agosti 30, mwaka huu Katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Best Art Promotion inayomsimamia bondia huyo, Makame Zumo alisema wameamua kumpeleka Cheka nje ya nchi, ili aweze kupata mazoezi ya kutosha na kujiweka sawa kwa ajili ya pambano hilo muhimu.


Zumo alisema kwa kushirikiana na kocha wa Cheka, Saleh Abdallah wameamua kuweka kambi nchini Kenya kutokana na nchi hiyo kuwa na Gym zenye kiwango cha hali ya juu na kuwa na walimu wazuri wa mchezo wa ngumi.
Al i s ema wa n a u h a k i k a watamsaidia bondia huyo kufanya vyema katika pambano lake dhidi ya mpinzani wake Derick Findley kutoka nchini Marekani.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa kabla ya kupambana na bondia huyo kutoka Marekani, Cheka atapanda ulingoni Agosti 10, mwaka huu mjini Morogoro kucheza mechi ya kirafiki na bondia Chimwemwe kutoka nchini Malawi katika pambano la kirafiki la raundi kumi litakalosimamiwa na PST.
Naye Cheka, amewaomba mashabiki wa ngumi kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono katika mapambano yote mawili, ambayo amesema ni magumu kwake, ingawa ana uhakika ataibuka na ushindi.
Kwa upande wake Kocha, Abdallah 'Komando' alisema ameshamwandaa kikamilifu bondia wake kiufundi na kisaikolojia, ili kuhakikisha anaibuka na ushindi katika mapambano yote mawili.

No comments:

Post a Comment