16 July 2013

AZAM FC TAYARI KWA LIGI KUU


 Na Shufaa Lyimo
UONGOZI wa klabu ya Azam FC umesema kwa sasa timu yao inaendelea na mazoezi ya viungo 'gym' na ya uwanjani kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Akizungumza Dar es Salaam jana Msemaji wa klabu hiyo, Jaffari Idd alisema lengo la kuanza mazoezi mapema ni kuhakikisha wanatwaa ubingwa huo safari hii na si kuishia nafasi ya pili tena.
"Timu yetu inaendelea vizuri na mazoezi vijana wapo katika hali nzuri na wameahidi kurudi kivingine baada ya ligi kuanza," alisema Jafari.
Alisema upungufu ambao ulijitokeza msimu uliopita, benchi la ufundi linaendelea kuyafanyia kazi ili yasiweze kujirudia tena.
"Upungufu ambao ulijitokeza msimu uliopita naamini hauwezi kujitokeza tena kutokana na mazoezi wanayoyafanya," alisema

No comments:

Post a Comment