Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Airtel T a n z a n i a k w a
kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni
(UNESCO) wamezindua mradi wa kuwezesha redio za kijamii kwa kuwapatia vifaa vya
redio na kuwaunganisha na mitambo ya mawasiliano ili kuwafikia wananchi wa
pembezoni kwa urahisi zaidi.
Mradi huo wa
kipekee ulizinduliwa rasmi jana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu
Fabian Masawe ambaye aliwatia moyo Airtel na UNESCO kuendelea na moyo huo wa
kusaidia jamii kupitia redio zao za kijamii ambazo ndiyo zipo karibu na
wananchi wa vijijini.
Aidha,
aliwataka wananchi wa Karagwe kuitumia Redio Karagwe kwa maendeleo ya jamii na
kuendeleza shughuli zao za kiuchumi kwani zaidi ya watu takriban milioni mbili
sasa watafikiwa na mawasiliano ya Redio Fadeco na Redio Karagwe.
Akizungumza na
waandishi wa habari katika uzinduzi rasmi wa mradi katika Redio ya Fadeco
Karagwe, Meneja Mahusiano ya Kijamii, Hawa Bayumi alisema kwamba mradi huo kwa
kushirikiana na UNESCO utawanufaisha wa t u wa p emb e z o n i ambao radio za
kijammii (Community Radios) ndio kimbilio lao la karibu katika kupata habari na
taarifa mbalimbali.
Afisa mradi wa
habari na mawasiliano UNESCO Yusuph Al Amin alisema wana ushirikiano na radio
za jamii kama nane na leo tumeanza na radio ya
Fadeco ambapo maeneo mengine pia yatanufaika na mradi huo.
Kwa u p a n d e wa k e Mkurugenzi wa
radio FADECO Bw.Joseph Sekiku alisema aliwashukuru Airtel na UNESCO kwa
kuboresha ufanisi wa huduma za radio Karagwe sasa takribani watu wapatao zaidi
ya milioni 2 wanapata mawasiliano ya radio tofauti na ilivyokuwa awali.
Kupitia mradi huo kampuni ya Airtel imeweza kuwapatia modem na simcard
radio za kijamii ili kuwawezesha waandishi wao wa Habari kufanyakazi kwa
ufanisi na kuinua mawasiliano katika maeneo ya vijiini nchini
No comments:
Post a Comment