29 January 2013

Polisi Pwani yawashikilia wahamiaji haramu watano



Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia wahamiaji haramu watano wa nchi ya Ethiopia na Somalia kwa kuingia nchini bila kibali.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ulrich Matei alisema raia hao walikamatwa wakati wa msako wa kukamata wahamiaji haramu.

Kamanda Matei alisema kuwa, wahamiaji haramu hao walikamatwa Januari 23, mwaka huu huko Kitongoji cha Kibosha Kijiji cha Mapinga wilayani Bagamoyo.

“Wahamiaji haramu hao walikamatwa wakiwa wanasafirishwa kwenye gari namba T 371 BTL aina ya Noah,” alisema Kamanda Matei.

Alisema kuwa, gari hilo lilikuwa likiendeshwa na Bw.Evarist Mbilinyi (25) dereva wa Mwananyamala Jijini Dar es Salaam akisaidiwa na Omary Karim (28) fundi magari mkazi wa Magomeni Makuti wakielekea Ethiopia kupitia Bagamoyo.

Aliwataja wahamiaji hao kuwa ni Itemegen Wolde (20) mwanafunzi, Beyene Dutano (25), Aduel Ashebo (24) na Detene Bore (25) kutoka nchini Ethiopia na Abdirsa Abdilim (20) ambaye ni raia wa nchi ya Somali.

No comments:

Post a Comment