31 August 2012

MSIBA

Mwili wa aliyekuwa Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda, Mhashamu Pascal William Kikoti, ukiteremshwa na baadhi ya Mapadri jana katika Uwanja wa Ngege, mjini Mpanda, mkoani Katavi, tayari kwa mazishi ambayo yatafanyika kesho. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Bashe, Kigwangala watoleana bastola *Walikuwa wakirudisha fomu za NEC *Katibu CCM Nzega aamulia ugomvi



Na Allan Ntana, Nzega

KATIKA hali isiyo ya kawaida, wagombea wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, wanaowania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), wilayani hapa, wanadaiwa kutishiana bastola.

CCM: Tunaweza kuifuta CHADEMA *Wassira awaonya kutovuruga amani nchini


Na Raphael Okello, Bunda

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Bw. Stephen Wassira, amesema Serikali ina uwezo wa kumuomba Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Bw. John Tendwa ili akifute Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kama kitaendeleza siasa za kuvuruga amani ya nchi.

Ngulume afariki dunia




Stella Aron na Heri Shaaban

MWANASIASA mkongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya mbalimbali nchini kwa miaka 18, Bi. Hawa Ngulume, amefariki dunia jana asubuhi jijini Dar es Salaam.

HAWA NGULUME


Mahakama yawaachia wanafunzi 51 UDSM


Na Grace Ndossa

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jana imewaachia huru na kuwafutia mashtaka wanafunzi 51 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi ya kufanya mikusanyiko na maandamano bila kibali.

Kujisaidia porini marufuku kuanzia kesho


Na Stella Aron

MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imesema kuanzia kesho abiria na wamiliki wa mabasi yanayosafiri umbali mrefu ambayo yatakutwa porini wakichimba dawa (kujisaidia), watakamatwa na kuchukuliwa hatua.

KATUNI


Mshindi BSS kuzindua albamu Uwanja wa Fisi


Na Mwandishi Wetu

MSHINDI wa mashindano ya Bongo Star Search (BSS) 2009, Pascal Cassian anatarajia kuzindua albamu yake ya nyimbo za injili ya Yasamehe Bure  keshokutwa Uwanja wa Fisi.

Dstv waongeza chanel mpya



Na Victor Mkumbo

KAMPUNI ya Multichoice, imezindua baadhi ya Chanel mpya ambazo zitaanza kuonekana hivi karibuni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Ofisa Habari wa Dstv Tanzania Barbara Kambogi, alisema wameamua kuzindua chanel mpya ambazo zitawafanya wateja wao kuangalia burudani mbalimbali.

Redds Miss Mwanza, Mashariki kivumbi


Na Mwandishi Wetu

SAFARI ya kuwania taji la Redd’s Miss Tanzania 2012 inaendelea kushika kasi, ambapo leo kutafanyika mashindano ya kumsaka Redd’s Miss Mwanza na kesho Redd’s Miss East Zone atapatikana Morogoro.

WANYANGE

Wanyange wa Jiji la Mwanza wanao taraji kupanda jukwaani kesho Ijumaa Agosti 30, 2012 katika ukumbi wa Yatch Club jijini humo kuwania taji la REDD'S MISS MWANZA 2012 wakiwa katika pozi mbalimbali. Shindano hilo linataraji kuwakutanisha miamba wawili wa Miondoko ya pwani, Bibie Hadija Omar Kopa na mkongwe Mwanahawa Alli na mkali mwingine Bob Haisa.

Mwanemti kutupa karata leo PARALIMPIKI



Na Amina Athumani

MWAKILISHI wa Tanzania katika michuano ya Walemavu ya Olimpiki (PARALIMPIKI) iliyoanza juzi jijini London, Uingereza Zaharani Mwanemti, leo anaanza kutupa karata yake ya kwanza.

Gadna G Habash sasa kurindima Times FM



Na Mwandishi Wetu

KITUO cha Redio Times FM, kinachokuja kwa kasi nchini jana kimemtangaza rasmi mtangazaji maarufu nchini, Gadna G. Habash kujiunga nao baada ya kukaa nje ya ulingo kwa muda mrefu.

UTAMBULISHO


Gadna G Habash akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani Dar es Salaam jana. Wengine kushoto kwake ni watangazaji wenzake Scholastica Mazula, Clifford Ndimbo na Khadija Shaibu 'Dida'. Kulia ni Jabir Saleh. Picha kwa hisani ya bongostaz

CHANETA yafanikiwa kwa mara ya kwanza



Na Amina Athumani

CHAMA cha Netiboli Tanzania (CHANETA), kimesema kwa mara ya kwanza michuano ya Ligi Daraja la Kwanza imefanikiwa kukusanya timu nyingi zaidi, tangu kuanzishwa kwa chama hicho ikiwa ni pamoja na timu zote kulipa ada ya ushiriki.

Twite akata mzizi wa fitna *Atua Dar, atamba kufanya makubwa


Na Charles Lucas

HATIMAYE ile filamu ya beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite imemalizika jana baada ya kuwasili Dar es Salaam na kukata mzizi wa fitna.

NIMEKUJA

Beki mpya wa Yanga, Mbuyu Twite akiwasalimia mashabiki wa timu hiyo waliofika kumlaki katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere, Dar es Salaam jana. Katikati ni Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Selestine Mwesiga kushoto kwake ni mwanachama wa Yanga, Ahmed Seif 'Seif Magari'. (Picha na Charles Lucas)

Milovan: Sasa mina timu ya mashindano



Na Elizabeth Mayemba

KOCHA Mkuu wa Simba, Milovan Cirkovic amesema kwa sasa kikosi chake kipo tayari kucheza mechi yao ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam FC, kwa kuwa wachezaji wake wamezoeana na wanaelewana vizuri uwanjani.

30 August 2012

Kadinda kufanya vitu vyake New York


Na Mwandishi Wetu

MBUNIFU wa Tanzania, Martin Survivor Kadinda ‘Martin Single Button’ anatarajia kuonesha mavazi yake kesho nchini Marekani katika onesho la mavazi la New York Africa Fashion Week na Music on The Caltwalk (MOC).

MBUNIFU MARTIN SURVIVOR


Mtanzania atakiwa kucheza Ujerumani


Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Mpira wa Miguu cha Ujerumani (DFB), kimetuma maombi ya kupatiwa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa ajili ya mchezaji Robert Makanja, ili aweze kucheza nchini humo.

BURUDANI

Washiriki wa mashindano ya Miss Utalii Tanzania 2012, Wilaya za Ilala na Kinondoni wakiwa na mmoja wa wadhamini wao 'Secrets Lingerie', wakiwa kwenye ufukwe wa Msasani. Washiriki hao kwa pamoja wanajiandaa na mashindano ya kuwatafuta wanyange watakaokwenda kushiriki fainali za Taifa. Picha na blogu ya issamichuzi 

Kutambulisha mwanamuziki mpya kesho



Na Mwandishi Wetu

BENDI ya muziki wa dansi Mashujaa "Wana Kibega', kesho wanatarajia kufanya onesho maalumu kwa ajili ya kumtambulisha mwanamuziki mpya ambaye hata hivyo uongozi wa bendi hiyo haujaweka wazi bedndi atakayotokea.

Wawili 'wavuta mkwanja' Mwanza



Na Mwandishi Wetu, Mwanza

KAMPUNI ya vinywaji baridi ya Coca-Cola ya Nyanza Bottlers, imewazawadia washindi wa promosheni ya 'Vuta Mkwanja' zawadi ya fedha taslimu.

Serengeti Boys kuivaa Misri


Na Mwandishi Wetu

TIMU ya Taifa ya Tanzania chini ya miaka 17 (Serengeti Boys), itaivaa Misri kwenye raundi ya pili ya michuano ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za 10 za Afrika kwa vijana chini ya miaka 17, zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.

Kocha Yanga kuwekwa kiti moto



Na Zahoro Mlanzi

SIKU moja baada ya Kocha Mkuu wa timu ya Yanga, Tom Saintfeit kudaiwa kusema hajatimiziwa baadhi ya vitu katika mkataba wake na kutishia kuondoka, uongozi wa Yanga umekuja juu na kusema utamchunguza kocha huyo kutokakana na kauli alizozitoa kama ni za kweli na kisha kuangalia vitu gani ambavyo hawajamtimizia.

29 August 2012

JK aomboleza vifo vya askari watatu JWTZ


Na Mwandishi Wetu

AMIRI Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya  Kikwete, ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, kuomboleza vifo vya askari watatu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliokuwa wanalinda amani Darfur, nchini Sudan, ambavyo vimetokea mwishoni mwa wiki iliyopita.

KATUNI


Mfadhili CHADEMA ahamia CCM



Na Faida Muyomba, Sengerema
 
MLEZI na Mfadhili Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Jimbo la Sengerema, mkoani Mwanza, Bw. Alex Manji, ametangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Polisi waua majambazi 4 Tabora


Na Frank Geofray, Jeshi la Polisi Tabora

JESHI la Polisi mkoani Tabora, limewaua majambazi wanne katika mapambano ya kurushiana risasi kati yao na polisi baada ya jaribio lao la kutaka kuvamia Congres Centre, kuzuiwa na jeshi hilo.

Washtakiwa wamkataa Hakimu


Na Rehema Mohamed

WASHTAKIWA wa kesi ya unyang'anyi wa kutumiwa siraha, jana wamemkataa Hakimu Waliyarwande Lema, anayesikiliza kesi hiyo kwa madai ya kutokuwa na imani naye.

SHANGA


Mwanamke mwenye asili ya kimasai anayeuza dawa za asili na shanga za urembo akipanga bidhaa hizo kwenye uzio wa Kituo cha Afya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. jamii hiyo awali ilikuwa ikijihusisha na ufugaji. (Picha na Charles Lucas)

Madaktari 50 kutoka India kutoa tiba Dar


Na Salim Nyomolelo

JOPO la madaktari 50 kutoka nchini India, wanatarajia kufanya maonesho ya matibabu katika ukumbi wa Diamond Jubilee Agosti 30 hadi 31, mwaka huu, kuanzia saa nne asubuhi hadi 11 jioni.

Kagasheki asikitishwa idadi ndogo ya watalii nchini


Na Mariam Mziwanda

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amesema idadi ndogo ya watalii wanaotembelea vivutio vingi vilivyopo nchini hairidhishi hivyo kuitaka sekta binafsi kuwa mhimili wa utalii nchini.

WAZIRI

Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki akizungumza na Wadau wa Utalii (Hawapo pichani), Dar es salaam jana, jinsi ya kukuza utalii nchini. (Picha na Sittu Athuman)

Mrema azidi kumshtaki Kimaro


Na Gift Mongi, Moshi

MBUNGE wa Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), Bw. Augustine Mrema, ameendelea kumshtaki kwa wananchi mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Bw. Aloyce Kimaro (CCM), kwa madai ya kupora ardhi zaidi ya ekari 10, zilizopo katika Mji Mdogo wa Himo wakati wa uongozi wake.

Jengo la Utawala Mombo laungua



Na Yusuph Mussa, Korogwe

JENGO la Utawala la Mamlaka ya Mji Mdogo Mombo, Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, juzi usiku limeteketea kwa moto pamoja na nyaraka zote za Idara ya Fedha, Masjala, Ofisi ya Mtendaji wa Mamlaka hiyo na Mwenyekiti wake.

Maziwa


Mfanyabiashara ndogo ndogo, akisukuma Baiskeli yake kwenye mitaa ya Jiji la Dar es Salaam jana, wakati akitembeza maziwa ya mtindi, juisi na maji. (Picha na Nyakasagani Masenza)

Mwakyembe ataka uundwaji tume kuboresha usafiri wa reli



Na Stella Aron

TANZANIA inakabiliwa na hali mbaya ya usafiri wa reli hivyo Serikali inapaswa kuunda kamati ambayo itatoa mapendekezo yatakayoboresha usafiri huo nchini.

Mwenyekiti wa Kamati ya Marekebisho ya Sera ya Usafirishaji nchini, Mhandisi Malima Bundala, aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya Waziri wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, kufungua warsha ya siku mbili kwa kamati hiyo.

Elimu ya kujitambua itakomesha tatizo la mimba kwa wanafunzi


TATIZO la mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini, linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya elimu.

Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinathibitisha kuwa tatizo hili limekuwa likiongezeka siku hadi siku hasa baada ya kuanzishwa shule za kata.

UKAGUZI


Baadhi ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, wakiwa kando ya Barabara ya Msimbazi, Kariakoo katika harakati ya kuuza Maji ya Vifuko, Jijini Dar es salaam. (Picha na Sittu Athuman)


Ushuru utumike kuboresha miundombinu sokoni



Na Lulu Malenda

MIUNDOMBINU ni sekta muhimu inayotakiwa kupewa kipaumbele ili kuongeza kasi ya maendeleo.

Nchi zilizoendelea zimewekeza katika miundombinu ambayo ndio kitovu cha sekta zote kwani kila kitu hutegemea usafiri ili kufika sehemu husika.

Malinzi kuzindua Rock City Marathon


Na Mwandishi wetu

MICHUANO ya mbio za Rock City Marathon 2012, inatarajia kuzinduliwa leo jijini Dar es Salaam.

Mbio hizo zitanduliwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Taifa Deoniz Malinzi na baadae washiriki watapata fursa ya kujaza fomu za maombi ya kushiriki.

KATUNI


Ghana, Niger mabingwa Rising Stars



NAIROBI, Kenya

FAINALI za michuano ya Airtel Rising Stars Afrika, zimefikia mwisho huku timu ya wavulana ya Niger na wasichana kutoka Ghana, zikinyakua ubigwa.

Michuano ya Tusker 'kutumbua' dola 450,000



Na Zahoro Mlanzi

KAMPUNI ya Bia Afrika Mashariki (EABL), imedhamini mashindano ya Kombe la Tusker kwa dola 450,000 yatakayofanyika nchini Uganda kuanzia Novemba 24 mpaka Desemba 8.

MAPOKEZI


Mmoja wa mashabiki wa Yanga waliofika kuilaki timu hiyo Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam juzi, wakati ikitokea Rwanda kwa ziara ya kimichezo kwa mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame akipokea Kombe la Kagame mara baada ya kuwasili. (Picha na Situ Athuman)

Uongozi Yanga wamruka Saintfeit *Ujio wa Twite giza totoro


Na Zahoro Mlanzi

SIKU moja baada ya Kocha Mkuu wa timu ya Yanga, Tom Saintfeit kutangaza kuwepo na mechi mbili za kirafiki, timu hiyo imemruka kimanga kocha huyo kwa kusema mechi wanayoitambua ni dhidi ya Coastal Union itakayocheza Jumamosi kwenye Uwanja Taifa, Dar es Salaam.

Filamu ya Yondan, Redondo kumalizika Jumapili



Na Zahoro Mlanzi

SAKATA la wachezaji Kelvin Yondan wa Yanga na Ramadhan Chombo 'Redondo' wa Simba, linatarajiwa kufikia tamati Jumapili baada ya Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake, Alex Mgongolwa kukutana kupitia usajili wa wachezaji kwa msimu wa 2012/2013.

28 August 2012

CCM: Hatuiombi radhi CHADEMA *Nape asisitiza ushahidi wa kutosha upo *Wajipanga kumfikisha Dkt. Slaa kortini



Na Salim Nyomolelo

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimewataka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwenda mahakamani haraka badala ya kusubiri kuombwa radhi ili kusafishwa dhidi ya madai ya chama hicho kupewa fedha na mataifa tajiri.

KERO YA MAJI


Mkazi wa Kijiji cha Matilinya, Kata ya Kwadelo, Jimbo la Kondoa Kaskazini, Bi. Esther Khamis, akichota maji kwenye dimbwi ambalo pia ng'ombe wanakunywa maji kama alivyokutwa  mwishoni mwa wiki, tatizo la maji kwenye eneo hilo linatokana na uchakavu wa miundombinu iliyojengwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere alipofanya ziara mwaka 1973. (Picha na Charles Lucas)

Mwanafunzi mbaroni kwa kupinga sensa


Na Anneth Kagenda

JESHI la Polisi nchini linamshikilia mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Bw. Yusuf Ernest, mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam kwa tuhuma za kusambaza ujumbe kwenye simu za mkononi ili kuhamasisha wananchi wasijitokeze kuhesabiwa katika Sensa ya Watu na Makazi iliyoanza Agosti 26 mwaka huu.

Sera za kibenki zinazotungwa zitekelezwe kwa vitendo



Na Cornel Antony

UMASKINI uliokithiri na hali ngumu ya maisha nchini umesababisha wananchi wengi kuwa waoga na kukosa ubunifu ili kujikwamua na hali hiyo.

Pia, wengine huogopa kukopa fedha katika taasisi za fedha ili kuanzisha miradi kwa kukosa ufahamu wa mikopo.

CRDB BANK

Mkuu wa Wilaya ya Masasi Bi. Farida Mgomi akifungua akaunti ya Malkia katika tawi jipya la benki ya CRDB   Wilayani Masasi hivi karibuni.

Zao la pareto likiangaliwa upya litakuwa mkombozi kwa wakulima



Na Alfred Mwahalende

LICHA ya kilimo kuwa ni uti wa mgongo kwa watanzania wengi
bado kuna kusuasua kwa sera na utekelezaji wa mipango na mikakati inayohusu sekta hiyo.

Jitihada zinahitajika kuukomboa ushirika Mtwara


Na Cornel Antony

SHERIA ya ushirika ni mwongozo uliopo kisheria ambao umepitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kupewa kibali kwa kusainiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

USAFIRI


Vijana wa Kijiji cha Nkuhi Kata ya Isuna, Mkoa wa Singida, wakisafiri kwa baiskeli huku mmoja wao akiwa amelala katika mwamba, hali hilo inatokana na shida ya usafiri katika eneo hilo. (Picha na Prona Mumwi)

Na Rehema Mohamed

BARAZA la Vyuo Vikuu Afrika Mashariki (IUCEA), limesema kuwepo ulinganifu wa elimu zinazotolewa katika vyuo vikuu vya nchi hizo, utawezesha wahitimu wa vyuo hivyo kupata kazi kwa unafuu katika nchi zote za Afrika Mashariki.

Askari wanyamapori wadaiwa kupora fedha zaidi ya mil. 4/-


Na Said Njuki, aliyekuwa Kondoa

WAFANYABIASHARA watatu wakazi wa Kijiji cha Itolwa, Wilaya ya Kondoa, mkoani Dodoma, wameiomba Serikali kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria askari sita wa Pori la Akiba  Mkungunero, kwa madai ya kuwateka, kuwatesa pamoja na kuwapora zaidi ya sh. milioni nne.

USAFI


Tingatinga la Manispaa ya Ilala, likisafisha uwanja kwenye Mtaa wa Mchikichini, Dar es Salaam jana, ili uweze kutumika katika shughuli mbalimbali za kijamii. (Picha na Anna Titus)

DC apoteza msafara wa Mwenge



Na Salma Mrisho, Geita

KATIKA hali isiyo ya kawaida, mbio za Mwenge wa Uhuru wilayani Geita, juzi ziliingia dosari baada ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Manzie Mangochie, kuupoteza msafara wake.

Hali hiyo ilikwamisha ukaguzi wa miradi iliyokuwa ikaguliwe na Kiongozi wa mbio hizo kitaifa, Kapteni Honest Mwanossa.

SUMATRA kukusanya maoni ya wadau kuhusu kanuni za usafirishaji



Na Grace Ndossa

MAMLAKA ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), leo itakutana na wadau wa sekta ya usafirishaji abiria kwa njia ya barabara, na wananchi ili kukusanya maoni yao kuhusu mapitio ya kanuni za ufundi, usalama na viwango vya ubora wa huduma kwa magari ya abiria.

'Mamlaka ziingilie kati ubora wa mafuta'


Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA zinazohusika kusimamia ubora wa mafuta ya petroli, zimetakiwa kuingilia kati na kutoa majibu sahihi ili kuondoa mkanganyiko ulioibuliwa na Shirika la Viwango nchini (TBS).

Mkanganyiko huo unatokana na TBS kutangaza kuwa, mafuta yanayotumika nchini yanaruhusiwa kuchanganywa na kemikali nyingine ikiwemo ethanol.

MAJI


Wakazi wa Kigamboni Kisiwani, wakijaza maji katika madumu kama walivyokutwa na mpigapicha wetu Dar es Salaam jana, tatizo la maji kwenye eneo hilo linasababisha kuuzwa dumu moja kwa sh. 200 hadi 500. (Picha na Sittu Athumani)

Halmashauri ziwe makini na fedha za miradi - RC



Na Agnes Mwaijega

HALMASHAURI zote jijini Dar es Salaam, zimetakiwa kuwa makini na usimamizi wa fedha na miradi ya maendeleo kwa kuhakikisha zinafuata sheria ya manunuzi na malipo.

ADC kupata cheti usajili wa kudumu



Na Rehema Maigala

CHAMA Kipya cha Siasa nchini, Alliance for Democratic Change (ADC), leo kinatarajia kupata cheti cha usajili wa kudumu baada ya kumaliza uhakiki wa wanachama katika mikoa 10 ya Tanzania Bara na Zanzibar.

DAWA


Mfanyabiashara wa kuuza dawa za kuua wadudu akitafuta wateja kama alivyokutwa Barabara ya Samora na Azikiwe, Posta Dar es Salaam jana. Uuzaji wa dawa hizo bila utaratibu maalumu ni hatari. (Picha na Heri Shaaban)

Hukumu ya Mtikila yasogezwa mbele


Na Rehema Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana  imesogeza mbele hukumu ya kesi ya kuchapisha na kusambaza walaka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, hadi Septemba 6 mwaka huu.

TFDA yaandaa mafunzo wataalamu wa maabara


Na Heri Shaaban

MAMLAKA ya Chakula na Dawa nchini (TFDA), jana imezindua mafunzo ya siku tatu ya wataalamu wa maabara kutoka nchi 13 za Afrika ambayo yameandaliwa na mamlaka hiyo.

HATARI


Gari Toyota namba T 145 ARU, likipita kando ya tawi la mti lililowekwa katika chemba ya maji ikiwa ni tahadhari kutokana na kutokuwapo mfuniko, kama lilivyokutwa makutano ya Barabara za Ohio na Samora, Dar es Salaam jana, mifuniko imekuwa ikiibwa na watu wasiofahamika na kuuzwa kama chuma chakavu. (Picha na Charles Lucas)

Wanne wafariki katika matukio tofauti Dar



Neema Kalaliche na Mariam Said

WATU wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti yaliyotokea jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na gazeti hili, Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela, alisema katika tukio la kwanza, mtoto Yaisi Mohamed (6), alikufa papo hapo baada ya kukanyagwa na gari wakati dereva wake akilirudisha nyumba bila kumuona.

'Wapuuzeni watu, vikundi vinavyotaka kukwamisha sensa'


Tumaini Maduhu na Andrew Ignas

MKUU wa Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, Bi. Regina Mgema, amewataka wananchi wilayani humo kuwa makini na kuwapuuza watu au vikundi vinavyoshawishi wasishiriki Sensa ya Watu na Makazi ili Serikali ishindwe kupanga mikakati ya maendeleo.

TUMEREJEA

Mshambuliaji wa Yanga Hamis Kiiza (katikati) akizungumza na mmoja wa mashabiki wa timu hiyo (kulia), ambao walijitokeza kuipokea timu hiyo iliyokuwa ikitokea Kigali,Rwanda katika ziara ya kimichezo. (Picha na Sittu Athuman)

Yanga yatua nchini bila Twite *Kutua leo kuikabili Mafunzo



Na Zahoro Mlanzi

MABINGWA wa Kombe la Kagame, Yanga wametua nchini jana wakitokea Rwanda huku Kocha Mkuu wa timu hiyo, Tom Saintfeit akimsifia beki wake mpya, Mbuyu Twite kutokana na uwezo aliouonesha na ametamba atamuanzisha katika mechi ya kesho dhidi ya Mafunzo ya Zanzibar.

27 August 2012

SENSA


Rais Jakaya Kikwete ( mbele katikati) akiwa na mkewe Mama Salma (mbele kulia) pamoja na familia yake akijibu maswali kutoka kwa Karani wa Sensa ya Watu na Makazi, Bw. Clement Ngalaba, Ikulu Dar es Salaam jana. (Na Mpigapicha Wetu)

Pinda awaondoa hofu wenyeviti *Makarani Ilala wagomea sensa hadi kieleweke



Na Mwandishi Wetu, Katavi

WAZIRI Mkuu, Bw.Mizengo Pinda, amesema posho za wenyeviti wa vitongoji na vijiji ambao wataambatana na makarani wa Sensa ya Watu na Makazi iliyoanza jana, zipo palepale hivyo hakuna sababu ya kujenga hofu juu ya malipo yao.

Karani wa sensa auawa, aporwa fedha sh. 200,000



Na Patrick Mabula, Kahama

KARANI wa sensa ambaye ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Kawe, iliyopo Kata ya Kilago, Wilaya ya Kahama, mkoani Shinyanga, Stanley Mahene, ameuawa na watu wasiofahamika na kuporwa sh.200,000, alizolipwa baada ya kuhudhuria mafunzo ya sensa.

NMB


Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ligula, iliyoko mkoani Mtwara wakisoma majarida ya Benki ya NMB Financial Fitness waliyogawiwa na wafanyakazi wa benki hiyo juzi, ili kujifunza shughuli za benki hiyo. (Na Mpigapicha Wetu).

Gharama elekezi za Sekta ya Ulinzi Binafsi


Na Mwandishi Wetu

CHAMA cha Sekta ya Ulinzi Binafsi nchini (TSIA), kimetangaza viwango vipya vya gharama elekezi kwa shughuli za ulinzi wa kampuni binafsi zinazotumia kiwango cha mshahara sh.80,000.

DC Lushoto ahadharishwa na wananchi



Na Yusuph Mussa, Lushoto

BAADHI ya wakazi wa Kata ya Vuga, Wilaya ya Lushoto, mkoani Tanga, wamesema Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw.Majjid Mwanga hatafanikiwa kuzuia uharibifu wa mazingira na uvunaji haramu wa mazao ya misitu, kama wenyeviti na watendaji wa vijiji katika kata hiyo wataendelea kubaki madarakani.

KUVUNJA SHERIA BARABARANI



Mwendesha pikipiki maarufu kama bodaboda jijini Dar es Salaam, ambaye jina lake halikufahamika akiwa chini ya ulinzi baada kukamatwa na askari akidaiwa kuvunja sheria za usalama barabarani katika Barabara ya Uhuru, mwishoni mwa wiki. (Picha na Anna Titus).

Serikali yadaiwa kutelekeza watu 5,000


Na Said Njuki, Babati

ZAIDI ya wakazi 5,000 wa Vijiji vya Ayamango, Gedamar na Gejedabugh, Wilaya ya Babati, mkoani Manyara, wanadaiwa kutelekezwa na Serikali wakidaiwa kuishi ndani ya eneo la Hifadhi ya Taifa Tarangire, iliyopo chini ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), kinyume cha sheria kwa zaidi ya miaka 50.

Mbinu za kuondokana na msongamano, foleni Dar


Na Mwandishi Wetu

TATIZO la msongamano wa magari katika barabara mbalimbali jijini Dar es Salaam, limekuwa likiongezeka siku hadi siku.

MIKOPO


Baadhi ya Wakulima wa Vijiji vya Kwadelo, Matilinya na Kelelechang'ombe, Kata ya Kwadelo, Jimbo la Kondoa Kaskazini, mkoani Dodoma, wakiangalia baadhi kati ya matrekta 64 aina ya Farmtrac kwenye viwanja vya hadhara juzi, waliyokopeshwa ili kutekeleza mpango wa Kilimo Kwanza kwenye kata hiyo. (Picha na Charles Lucas)

Waliomliza DC Nkasi kamwe wasichekewe, wachukuliwe hatua



MWISHONI mwa wiki, Mkuu wa Wilaya ya Nkasi, mkoani Rukwa, Bw. Idd Kimanta, aliangua kilio kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani mjini Namanyere, baada ya kusikitishwa na utendaji mbovu wa Mkurugenzi pamoja na Wakuu wa Idara mbalimbali.

Serikali kuwafikishia huduma za simu wananchi-Dkt.Mgimwa


Na Eliasa Ally, Iringa

WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Dkt.William Mgimwa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kalenga mkoani Iringa amesema Serikali itahakikisha wananchi ambao hawafikiwi na mawasiliano ya simu za mkononi hususan katika maeneo ya vijijini inawajengea minara.

Mtoto anusurika kuibwa



Na Mwandishi Wetu, Bukoba

MTOTO wa miaka miwili na nusu, Vanesa Victor, amenusurika kuibwa na watu wasiojulikana waliofika nyumbani kwao wakiwa ndani ya teksi na kumtaka apande ili wampatie soda.

BURUDANI

Wasanii wa Kikundi cha Kwaya cha The Tanzanite Eagles cha Benki ya Barclays, wakifanya onesho maalumu kwenye ukumbi wa Kituo cha Utamaduni cha Urusi, Dar es Salaam juzi, wakijiandaa kwa safari ya Afrika Kusini, ambako watashiriki onesho la kwaya kwa vikundi vya nchi za Afrika. (Na Mpigapicha Wetu)

DAAA yatamba kung'ara mashindano ya Taifa



Na Amina Athumani

CHAMA cha Riadha Mkoa wa Dar es Salaam (DAAA), kimetamba kufuta uteja katika mashindano ya Taifa ya mchezo huo na kwamba watahakikisha wanavunja rekodi kwa mkoa huo.

Miss East Afrika sasa kufanyika Des. 7


Na Neema Kalaliche

MASHINDANO ya Miss East Afrika kwa mwaka huu, yamepangwa kufanyika Desemba 7 badala ya Septemba katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam na yanatarajiwa kurushwa 'live' kupitia M-Net.

KATUNI


Nyota wa kikapu NBA akoshwa na vipaji nchini



Na Amina Athumani

NYOTA wa timu ya mpira wa kikapu ya Chicago Bulls inayocheza Ligi Kuu ya mchezo huo Marekani (NBA), Luo Deng ameridhishwa na uwezo wa chipukizi wa Tanzania baada ya kuwaona katika kliniki inayoendeshwa na Mtanzania, Hashim Thabit anayechezea ligi hiyo pia.

Simba yazuru TBL Arusha


Na Mwandishi Wetu, Arusha

TIMU ya Simba ambayo imeweka kambi mkoani Arusha,   imefanya ziara ya kutembelea Kiwanda cha kutengeneza Bia Tanzania (TBL) kilichopo jijini hapa.

TBL

Mratibu wa Usalama na Afya wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kassena Heavy (kushoto), akiwaeleza jambo wachezaji na viongozi wa Klabu ya Simba waliotembelea Kiwanda cha TBL kilichopo Arusha mwishoni mwa wiki, ili kujionea uzalishaji wa bia ya Kilimanjaro Lager ambayo ndio mdhamini wao mkuu. (Picha na Executive Solutions)

BFT yaomba maandalizi mapema Olimpiki 2016



Na Amina Athumani

SHIRIKISHO la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT), limeiomba Serikali kuanza maandalizi mapema ya Michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016 itakayofanyika nchini Brazil, ili kuepuka kujirudia kufanya vibaya kwenye michezo hiyo.

Tanzania yatoka kapa Zone 5 kikapu



Na Amina Athumani

TIMU za Tanzania zilizokuwa jijini Kampala, Uganda kwenye mashindano ya Zone 5, yanayoandaliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Kikapu (FIBA), zimeondoshwa kwenye michuano hiyo.

Timu hizo ni ABC na Savio kwa timu za wanaume na Jeshi Stars na Don bosco kwa timu za wanawake.

MAADHIMISHO


Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim, Bw. Yogesh Manek  akishikwa mkono na moja wa wakurugenzi wa Bodi ya benki hiyo, Bw. Juma Mwapachu (kushoto), wakati wa sherehe ya  wafanyakazi kuadhimisha, Miaka 15 tangu kuanzishwa iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, (Wa pili kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Bw. Anthony Grant. (Na Mpigapicha Wetu)

Yanga we acha tu Kigali *Yaichapa Polisi 2-1 *Simba anguruma Arusha


Na Zahoro Mlanzi

MABINGWA WA Kombe la Kagame, timu ya Yanga, imeendeleza wimbi la ushindi katika kambi iliyoweka jijini Kigali baada ya kuichapa Polisi Force ya jini humo kwa mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa uliopigwa kwenye Uwanjwa Stade de Kigali.

Watoto wa kike watakiwa kujitambua



Na Victor Mkumbo

WANAWAKE wenye umri chini ya miaka 18, wametakiwa kujitambua ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea.

Akizungumza katika Semina ya waschana wenye umri wa kuanzia miaka 11 mpaka 18 juzi, Mkurugenzi wa Shirika la TWA, Irene Kiwia alisema kuwa vijana wanatakiwa kujitambua ili kuweza kufikia malengo.

Polisi wafichua hujuma ya sensa *Wabaini uwepo wa kikundi kilichopanga kuivuruga


Stella Aron na Anneth Kagenda

JESHI la Polisi nchini limedai kubaini uwepo wa kikundi cha watu ambao wanajipanga kuvuruga Sensa ya Watu na Makazi ambayo imepangwa kuanza usiku wa kuamkia Agosti 26 mwaka huu.

Katibu CHADEMA Morogoro ajiuzulu


Na Lilian Justice, Morogoro

KATIBU wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mkoani Morogoro, Bw. Abeli Luanda, jana ametangaza kujiuzulu wadhifa huo kwa madai ya kutoridhishwa na utendaji mbobu wa chama hicho ngazi ya Mkoa na Taifa.

Dkt. Slaa amtuhumu Kikwete




Na Goodluck Hongo, Morogoro

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kusaini posho, marupurupu ya wabunge na kushindwa kuongeza mishahara ya watumishi wa kada nyingine, kinaweza kuing'oa Serikali yake madarakani.

CUF: Siasa chafu Arusha hatuzitaki



Na Said Njuki Arusha

CHAMA Cha Wananchi (CUF) mjini Arusha, kimewataka wakazi wa jiji hilo kuwa makini na siasa za kupakana matope ambazo haziwezi kuleta tija katika maisha yao.

Wavuvi waokolewa Z'bar, mmoja afariki dunia



Na Mohammed Mhina, Jeshi la Polisi Zanzibar

WAVUVI wawili raia wa nchi jirani ya Komoro, wameokolewa kwenye kisiwa kidogo cha Pungume, nje kidogo ya Zanzibar wakiwa hoi kutokana na uchovu, njaa baada ya kupotea baharini siku 11 bila kula chakula wakiwa na boti ndogo ambayo iliishiwa mafuta.

24 August 2012

Mwakyembe aibua ufisadi bandarini *Mkurugenzi Mkuu asimamishwa kazi na wengine watatu *Kisa utendaji mbovu, wizi, rushwa, uchunguzi waendelea


Na Agnes Mwaijega

WAZIRI wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, ameiagiza Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA), kuwasimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo Bw. Ephrahim Mgawe na wasaidizi wake watatu kwa tuhuma za wizi, rushwa na utendaji mbovu.

MWEKYEMBE


Waziri wa Uchukuzi, Dkt Harrison Mwakyembe akitoa tamko la kuwasimamisha kazi baadhi ya Watendaji wa Mamlamka ya Bandari Tanzania (TPA) kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)Dar es Salaam jana, hatua hiyo imechukuliwa kufuatia tuhuma za wizi, rushwa na utendaji mbovu. (Picha na Heri Shaaban)

Mramba akiri kutoa msamaha



Na Grace Ndossa

ALIYEKUWA Waziri wa Fedha, katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Bw. Basil Mramba, amekiri kutoa msamaha wa kodi kwa Kampuni ya Alex Stewart, iliyoletwa na Serikali ili kufanya ukaguzi wa hesabu katika migodi ya dhahabu nchini kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za mkataba.

Papaa Msofe aumwa, kesi yaahirishwa



Na Grace Ndossa

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana imeshindwa kusikiliza kesi inayomkabili mfanyabiashara maarufu jijini hapa, Bw. Marijani Msofe (50), maarufu 'Papa Msofe', kwa sababu mshtakiwa anaumwa.

USAFI


Wafanyakazi wa usafi wa Manispaa ya Ilala  wakifagia barabara ya Azikiwe kama walivyokutwa na mpiga picha wetu  juzi, Jijini Dar es Salaam(Picha na Mpiga Picha Wetu)

Machinga Complex wamjibu Masaburi



Na Zourha Malisa

BODI ya Wakurugenzi Jengo la Machinga Complex, imeshtushwa na taarifa iliyotolewa na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dkt. Didas Masaburi, kuwa Jiji hilo linakusudia kumuomba Rais Jakaya Kikwete, aruhusu jengo hilo lichukuliwe na Serikali.

Mishahara ya walinzi sekta binafsi yapanda



Jesca Kileo na Darlin Said

CHAMA cha Sekta ya Ulinzi Binafsi nchini (TSIA), kimetangaza viwango vipya vya mishahara ya walinzi wa kampuni binafsi ambayo imepanda kwa zaidi ya asilimia 100.

HATARI

Abiria na mzigo wa pikipiki wakiwa wambebwa kwenye baiskeli ya miguu mitatu, maarufu kama guta, kitendo ambacho kinahatarisha usalama wa watumiaji barabara hivi karibuni kama walivyokutwa hivi karibuni katika barabara ya zamani ya Bagamoyo maeneo ya Mlalakua. (picha na Anna Titus)

Muhongo: Tutaendelea kusafirisha mchanga wa dhahabu nje ya nchi


Na Raphael Okello, Bunda

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema Serikali itaendelea kusafirisha mchanga ya madini nje ya nchi ili ukafanyiwe uchunguzi kutokana na ukosefu wa maabara zenye uwezo wa kubaini aina mbalimbali za madini nchini.

Hakimu akwamisha kesi ya kusafirisha binadamu Yemen



Na Grace Ndossa

KESI inayohusu biashara haramu ya kusafirisha binadamu nchini Yemen inayomkabili mfanyabiashara mkazi wa Arusha, Bw. Salim Ally, imeahirishwa kwa sababu hakimu anayeisikiliza Bw. IIvin Mgeta, kupata udhuru.

Kagasheki aongeza uwazi Malisili



Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amebadili taratibu za kuwapata wajumbe wa bodi mbalimbali zilozopo chini ya Wizara hiyo.

Ajali


Vijana ambao hawakuweza kupatikana majina yao mara moja wakiondoa mbao zilizoelemea mkokoteni katika barabara ya Sokoine, Dar es Salaam hivi karibu kama walivyokutwa na kamera yetu. (Picha na Sittu Athmani)

Majenerali watatu JWTZ kuagwa leo



Na Mwandishi Wetu

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), leo litawaaga Majenerali wake ambao wamestafu jeshi kwa mujibu wa sheria.

NBC kutumia fursa za kiuchumi kupiga hatua


Na Godfrey Ismaely

BENKI ya NBC, imesema licha ya changamoto zilizopo katika ushindani wa kibiashara na uwekezaji, bado kuna fursa nyingi za masoko ambapo hali hiyo inaweza kuifanya benki hiyo iweze kujiimarisha na kukua zaidi kibiashara nchini.

Ombaomba


Mwanamke anaeshi katika mazingira magumu akiwa na mtoto wake kando ya makutano ya Barabara ya Nyerere na Uhuru, Mnazi Mmoja wakiwa wakijiandaa na shughuli ya kuomba msaada kama walivyokutwa na kamera yetu jana, Dar es salaam jana.(Picha na Sittu Athuman)


Umakini wa makarani wa sensa utafanikisha kazi hiyo



Na Suleiman Abeid

AGOSTI 26, 2012 ni siku muhimu nchini kwa watanzania kutokana na sensa  yanye nafasi kubwa katika taifa, kwani itawezesha serikali kupanga bajeti kulingana na idadi ya watu.

Sensa imesubiriwa kwa kipindi kirefu ikiambatana na semina, mafunzo na hamasa kwa wananchi juu ya umuhimu wake kwa maendeleo ya Taifa.

Uboreshaji maduka ya dawa, kuimarisha afya za wananchi.


Na Willbroad Mathias

MAMLAKA ya Chakula na Dawa nchini(TFDA), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na shirika lisilo la kiserikali la Marekani la Management Science for Health (MSH), imekuwa ikitekeleza Mpango wa Kuboresha maduka ya dawa Baridi (DLDBs) ili yawe ya dawa Muhimu (ADDO).

Mpango huu umekuwa ukitekelezwa kupitia fedha za serikali na wafadhili na hadi sasa mikoa 18 kati ya 25 nchini imefikiwa na mpango huu.

KATUNI


Kingoile apeta usaili Kilimanjaro


Na Elizabeth Mayemba

ALIYEWAHI kuwa kiongozi wa zamani wa Klabu ya Villa Squad, Ally Kingoile amepita katika usaili wa wagombea uongozi katika Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kilimanjaro, ambapo anagombea nafasi ya Katibu Msaidizi.

Nyilawila ajichimbia Mbeya



Na Mwali Ibrahim

BONDIA Karama Nyilawila, ameamua kuhamishia kambi yake mkoani Mbeya akiwa na lengo la kujiandaa vizuri na pambano lake dhidi Francis Cheka.

UTAMBULISHO


Msanii wa muziki wa dansi nchini Kalala Junior (katikati), akicheza na baadhi ya wanenguaji wa bendi ya Twanga Pepeta wakati alipotambulishwa kujiunga na bendi hiyo Dar es Salaam jana. (Picha na Victor Mkumbo)

Kalala Junior arudi Twanga Pepeta



Na Zahoro Mlanzi

MSANII nyota wa muziki wa dansi nchini, Kalala Hamza 'Kalala Junior', amerejea katika bendi yake ya zamani, African Stars 'Twanga Pepeta'.

Msanii huyo ameamua kurudi rasmi katika bendi hiyo, baada ya kuondoka kwa miaka kadhaa ambapo alijiunga na bendi ya Mapacha Watatu.

AY, Papa Wemba, 2face jukwaa moja


Na Mwandishi Wetu

WANAMUZIKI nguli Afrika, wataungana na msanii mahiri wa kizazi kipya nchini Ambwene Yessaya, kutumbuiza wakati wa mechi ya fainali ya michuano ya Airtel Rising Stars, itakayopigwa kesho Uwanja wa Nyayo jijini Nairobi.

23 August 2012

Vunja na Vurugu


Baadhi ya wafanyakazi wa Yono Action Mart, wakivunja Nyumba namba 80 kwa amri ya Mahakama. Kuvunjwa kwa nyumba hiyo iliyoko Kongo na Mkunguni, kulizusha vurugu kubwa zilizosababisha Polisi kurusha mabomu ya machozi kutawanya watu, Dar es Salaam jana. (Picha Charles Lucas na Shufaa Lyimo)

Mramba amtaja Mkapa kortini *Ni katika kesi ya kutumia madaraka vibaya *Adai ndiye aliyebariki ujio Kampuni Alex Stewart *Chenge, Cheyo, Gavana kumtetea mahakamani


Na Grace Ndossa

ALIYEKUWA Waziri wa Fedha, Bw.Basil Mramba, anayekabiliwa na kesi ya kutumia vibaya madaraka na kuisababishia Serikali hasara ya sh.bilioni 11.7, ameanza utetezi wake ambapo amemtaja Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Bw.Benjamin Mkapa kuwa alibariki Kampuni ya Alex Stewart kuingia nchini.

Mchuano wa urais 2015 waibukia Hanang'


Na Mwandishi Wetu

KATIKA kile kinachohusishwa na urais wa mwaka 2015, hali ya kisiasa wilayani Hanang' mkoani Manyara imezidi kuwa tete huku kauli za wanasiasa vinara wilayani humo zikiibuka siku hadi siku.

KATUNI


CCM ijipange Igunga-Sitta *Ofisi ya Bunge yamlilia Dkt.Kafumu, NEC yanena



Na Waandishi Wetu

SIKU moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Tabora, kutengua matokeo ya uchaguzi ya Jimbo la Igunga, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Jimbo la Urambo mkoani Tabora kwa tiketi ya CCM, Bw.Samuel Sitta, amewataka wana-CCM kuheshimu uamuzi huo na kuendelea kujipanga.

DC Serengeti afariki, Rais Kikwete amlilia


Na Veronica Modest, Musoma.

MKUU wa Wilaya ya Serengeti, Bw.James Lyamungu, amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kutokana na kifo hicho, Rais Jakaya Kikwete, amemtumia Mkuu wa Mkoa wa Mara, Bw.John Tupa, salamu za rambirambi kuomboleza kifo cha Bw.Yamungu kilichotokea alfajiri ya jana MNH.

KATUNI